Wananchi
wilayani Karagwe wametakiwa kuendelea
kuvuta subira wakati
jitihada za kufuatilia vitongoji
na vijiji ambayo havikupata umeme
wa Rea zinaendelea
kufanyika ili kuhakikisha
awamu ya tatu
inayofuatia vinapata umeme
huo.
Kauli hiyo imetolewa
na mbunge wa Jimbo
la Karagwe Innocent
Bashungwa katika mikutano
ya hadhara ya
kuwashukuru wananchi kumchagua
pia kuwapa mrejesho
wa masuala mbalimbali ya maendeleo
alizoshghulikia kwa nafasi
yake ya uwakilishi
wa wananchi Bungeni.
Amesema
wizara ya Nishati
na madini kupitia
mradi wa umeme
vijijini tayari wamemuhakikishia kuwa
vitongoji na vijiji
vyote ambavyo havikupata
umeme huo kwa
awamu zilizopita hivyo
akasema kuwa tayari
ameorodhesha vitongoji na
Vijiji vilivyokosa umeme
huo na vimeisawailishwa kwa
waziri wa wizara
husika.
Katika hatua nyingine
Innocent Bashungwa amesema
mradi wa maji
wa Rwakajunju tayari
umetengewa fedha katika
bajeti ya mwaka 2016/2017 zimetengwa
dolla million 30
ambazo ni sawa na shilingi
billion 65 fedha
za kitanzania na
kusema ukikamilika utakuwa
ni mkombozi kwa
wananchi.
Mtendaji wa
Kata ya
Bweranyange Niclous
Rubambura akisoma taarifa
ya Kata amesema
kuwa inakabiliwa na
changamoto ya kutokuwa
na watendaji wa
vijiji hali inayosababisha kazi
za kuwaletea maendeleo
kwa wananchi kukwama.
Amesema kata hiyo
ina vijiji 4
lakini ni vijiji vitatu
havina watendaji na
kijiji kimoja cha
Chamchuzi mtendaji wake
ni mgonjwa wa
muda mrefu hivyo
ni changamoto kubwa.
Wananchi wa vijiji vya
kata ya Bweranyange
wamesema kuwa ili
kasi ya maendeleo
iwepo ni lazima watumishi
waliopo wasipewe majukumu
ambayo siyo utalaamu
wao kwani waliokaimu vijiji wengi
wao ni walimu.
Akijibu hoja hizo Mbunge wa jimbo la Karagwe Innocent Bashungwa amesema kuwa changamoto za upungufu wa watumishi katika wilaya ya Karagwe anazitambua.
Hata hivyo amewataka
wananchi kuchangamkia fursa
ya kuwa jirani
na Nchi ya
Rwanda na nchi
hiyo imeanzisha kiwanda
cha kutumia mihongo
hivyo wananchi wakalime
kwa wingi mihogo.
Post a Comment