Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: MAAGIZO NA MAELEKEZO YA WAZIRI WILLIAM LUKUVI KWA WATENDAJI WA SERIKALI MKOANI KAGERA
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akiwa Mkoani Kagera katika siku yake ya pili mara baada ya sik...




Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akiwa Mkoani Kagera katika siku yake ya pili mara baada ya siku ya kwanza kuitumia kutatua migogoro ya wananchi kuhusu ardhi siku ya pili ya tarehe 19.08.2016 aliitumia kuaongea na watendaji  mbalimbali wa Serikali akiwa mkoani hapa.


Eneo la kwanza aliloliongelea Mhe. Lukuvi ni kuhusu migogoro ya ardhi kwa wanachi  iliyo mingi ilisababishwa na Watendaji wa Serikali waliopewa dhamana ya kushughulikia suala la ardhi, ambapo aliwaonya Watendaji wote kuacha tabia hiyo mara moja. Agizo, aliwaagiza Makatibu Tawala wa Mikoa wote nchini kuwachukulia hatua za kinidhamu au kuwafukuza kazi  Watendaji hasa Maafisa Ardhi watakobainika kusababisha migogoro ya ardhi katika maeneo yao.



Katika Agizo hilo Mhe. Lukuvi alimpa Onyo kali Mthamini wa Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba Bw. Projestus Katabalo kuacha mara moja kufanya kazi kwa mazoea bila kufuata sheria, taratibu na kanuni za utekelezaji wa zoaezi la uthamini.






Eneo la pili, Mhe. Lukuvi alisema kuwa kupitia Wizara yake Serikali imepanga ndani ya miaka kumi kuwa itakuwa imepanga, imepima na kumilikisha ardhi yote ya Taifa la Tanzania. Agizo, Mhe. Lukuvi aliagiza Mikoa yote nchini kuanza kuweka mipango ya kupanga, kupima na kumilikisha ardhi. Aidha aliuagiza uongozi wa Mkoa wa Kagera kuhakikisha unatoa hati miliki elfu kumi za ardhi kwa mwaka huu wa fedha 2016/17ambapo lengo la kitaifa ni hati Laki nne.


Agizo la pili ni kuhusu kupima maeneo yote ya Serikali (Serikali za Mitaa na Serikali Kuu) pamoja na kubaini majengo yote ya Serikali ambapo yeye kama Waziri mwenye dhamana atatoa hati maalum yenye msamaha wa kodi ya kumiliki maeneo ya Serikali ili yaachwe bila kuingiliwa na wananchi.



Agizo la tatu, ni Maafisa Mipango Miji kuhakikisha wanaainisha maeneo yote yaliyoiva kuwa miji ili yapangwe, kupimwa na kumilikishwa kwa hati za muda mrefu badala ya hati za kimila. Agizo la nne ni maeneo yote ambayo wananchi walijenga miaka ya zamani na yapo katika miji (Makazi Holela) nyumba zisivunjwe bali wananchi Warasmishiwe makazi hayo kwa kuyapanga.



Eneo la Tatu aliloongelea Mhe. Lukuvi ni Kuhusu Migogoro Mikubwa  ambapo alisema kuwa katika migogoro hiyo mfano wakulima na wafugaji, alisema kuwa Serikali imeamua kuunda kamati ya Wizara nne ili kamati hiyo ipitie migogoro yote mikubwa  na kutoa ushauri kwa Mawaziri wa Wizara hizo husika ili kukomesha kabisa migogoro hiyo.


Wizara hizo nia Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Wizara ya Kilimo, Uvuvi na Mifugo, TAMISEMI, na Wizara ya Maliasili na Utalii.


Angalizo mikoa yote iliagizwa kuacha ugawaji wa Kata na Vijiji wakati wa Uchaguzi Mkuu bila kuihusisha Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwani mipaka inayotolewa na Mikoa inashindikana kuonana na mipaka ambayohupimwa  ardhini na Wizara ya Ardhi. Ili kusuluhisha hilo aliagiza Wizara yake kupewa taarifa pale Mikoa inapotaka kugawa maeneo yake lakini kwa sababu za msingi bila shinikizo la wanasiasa.




Katika kuhitimisha Mhe. Lukuvi alisema kuwa Wizara yake inatengeneza sera ya Ardhi, Nyumba na Makazi ambaop aliagiza Maafisa Mipango Miji wote nchini katika Halmashauri, Miji, Majiji, na Manispaa kuhakikisha wanaitisha vikao vya wadau ili kuamua aina ya rangi zipakwe katika miji badala ya kila nyumba kupakwa rangi yake na lengo ni kuifanya miji ipendeze kwa kuwa na mpangilio wa upakaji wa rangi.





Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu alimshukuru Mhe. Lukuvi kwa kufanya ziara yake Mkoani Kagera na kutatua kero mbalimbali za wananchi ambapo alimuhaidi Mhe. Lukuvi  kuwa maelekezoa na maagizo yake yote yatafanyiwa kazi  na wahusika ili kuhakikisha migogoro ya ardhi inakomeshwa Mkoani Kagera.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top