Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: WASHAURI VIPORO VYA MIRADI YA MAENDELEO VIKAMILISHWE KABLA YA KUANZA MIRADI
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
Baraza la   Madiwani katika halamashauri ya wilaya ya Misenyi wameiomba halmashauri ya Misenyi kwa kushirikiana na serikali kuu kumalizi...

Baraza la  Madiwani katika halamashauri ya wilaya ya Misenyi wameiomba halmashauri ya Misenyi kwa kushirikiana na serikali kuu kumalizia miradi ya maendeleo ambayo haikumalizika katika mwaka wa fedha 2015/2016.


Wakiwasilisha taarifa zao za utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika kata zao  mbele ya mwenyekiti wa halmashauri hiyo kipindi cha APR-JUN madiwani hao wamesema kuwa licha ya kuanza mwaka mpya wa fedha bado kunaviporo vingi vya miradi ya maendeleo ambavyo havikutekelezwa.


Miradi mikubwa ambayo iliwekwa kwenye bajeti na haikutekelezwa kwa asilimia kubwa ni pamoja na miradi ya ukarabati wa barabara zinazounganisha kata na vijiji ,miradi ya maji pamoja na ukarabati wa miundo mbinu hasa katika nyumba za walimu ,shule na vituo vya afya.


Akizungumzia swala la ukarabati na utengenezaji wa barabara katika kata mbalimbali  za halmashauri ya Missenyi mwenyekiti wa halmashauri hiyo PROJESTUS TEGAMAISHO amesema kuwa barabara zote zilizotengewa bajeti kupitia mfuko wa CBJ mfuko huo haukuleta fedha za barabara.


TEGAMAISHO amesema kuwa kutokana na viporo muhimu kutotekelezwa katika bajeti iliyopita wataendelea kushughulikia miradi hiyo na kuibua upya ili kuwaondolea wananchi adha inayowakabili.


Baadhi ya changamoto nyingine zilizotajwa na madiwani katika kata zao ni upungufu wa watumishi hasa maofisa watendaji wa vijiji upungufu wa madawa katika vituo vya afya upungufu wa walimu wa sayansi na upungufu wa nyumba za walimu na vyumba vya madarasa.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top