Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: WATAKIWA KUZINGATIA KANUNI ZA KILIMO ILI KUPATA MAZAO BORA YA JASHO LAO.
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
Wakulima wa zao la kahawa Wilaya ya   Karagwe Mkoani   Kagera wametakiwa kuzingatia kanuni za kilimo ili kuhakikisha wanavuna kah...



Wakulima wa zao la kahawa Wilaya ya  Karagwe Mkoani  Kagera wametakiwa kuzingatia kanuni za kilimo ili kuhakikisha wanavuna kahawa yenye ubora ambayo itawaongezea kipato chao.


Wito huo umetolewa na Afisa kilimo anayeshughulika na zao la kahawa Wilayani Karagwe Cleophace Kanjagaile leo wakati akiongelea  kuhusu utunzaji wa ubora wa kahawa.


Kanjagaile amesema wakulima wa zao la Kahawa wakizingatia kanuni za kilimo wanazoelekezwa na wataalamu wa kilimo anaamini zao hilo litakuwa la thamani sana kutokana na kuwa kila mmoja atakuwa anavuna kahawa yenye ubora.


Ameeleza kuwa kanuni za kilimo bora anazopaswa kuzingatia ni kuzingatia muda wa kupanda mche wa kahawa, hadi kufikia wakati wa kuvuna kahawa kwa kufuata taratibu zote zinazoelekezwa.


Pia Kanjagaile ameeleza kuwa  sasa msimu wa kuanza kuvuna kahawa mwaka huu umekaribia wakulima hawana budi kuhakikisha wanavuna kahawa iliyokomaa na kuianika sehemu nzuri kama ambavyo wamekuwa wanaelekezwa na wataalamu wa kilimo ili kupata bei nzuri ya zao hilo.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top