Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: WAHIMIZWA KUVUNA KAHAWA ILIYOIVA NA KUKOMAA KWA UBORA UNAOTAKIWA
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
Halmshauri ya wilaya ya Karagwe kupitia idara ya kilimo wametoa tahadhari kwa wakulima wilayani humu wanaojihusisha na vitendo ...





Halmshauri ya wilaya ya Karagwe kupitia idara ya kilimo wametoa tahadhari kwa wakulima wilayani humu wanaojihusisha na vitendo vya uvunaji wa kahawa mbichi na uuzaji wa kahawa za magendo (Ubutura) vitendo vinavyosababisha kukosa kahawa zenye ubora.

Afisa kilimo Mkaguzi wa Kahawa wilaya ya Karagwe Cleophace Kanjagaire amesema kuwa kwa sasa kuna baadhi ya maeneo wakulima wameanza kuvuna kahawa mbichi na kuuza magendo jambo ambalo amelitaja kuwa ni kunyume na sheria na atakayekamwa anafanya hivyo atachukuliwa hatua za kisheria ikiwemo kunyanganywa kahawa hizo na kulipa faini.

Kanjagaire amesema kuwa tayari watendaji wameshapewa barua za kuangalia suala laukaguzi na  udhibiti wa ubora wa kahawa katika maeneo yao na hilo linatakiwa kuzingatia na kuhakikisha hakuna mkulima anayevuna kahawa mbichi.

Ameongeza kuwa hakuna mkulima anayekatazwa kuvuna kahawa lakini anatakiwa avune zile zilizoiva kwani uvunaji wa kahawa mbichi unaharibu ubora wa kahawa na sheria inakataza vitendo hivyo.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top