Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: WALENGWA WA MPANGO WA TASAF 111 WILAYA YA KARAGWE WAPEWA ELIMU YA MATUMIZI
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
Watumishi   wa   serikali   waliopewa   jukumu la   kujaza   taarifa   za watoto    walio katika   mpango   wa   kunusuru   kaya   maski...

Watumishi  wa  serikali  waliopewa  jukumu la  kujaza  taarifa  za watoto   walio katika  mpango  wa  kunusuru  kaya  maskini  wa TASAF  III kuhakikisha  wanazijaza  kikamilifu  na  wale  ambao  wanakataa  kuzijaza kwa  kisingizio  cha  kutaka  kulipwa  posho  ya  kazi  hiyo  wametakiwa  kuripotiwa  mara  moja  ili waweze  kuchukuliwa  hatua  za  kinidhamu    dhidi  yao.



Kauli  hiyo  imetolewa  na  mwenyekiti  wa   halmashauri  ya  wilaya  ya  Karagwe  Wallesi  Mashanda  wakati  akitoa  elimu  na  hotuba  kwa  walengwa  wa  kunusuru  Kaya  maskini   wa  kijiji  cha  Kanoni   Kata  ya  Kanoni  ikiwa  ni  mwendelezo  wa   kamati  ya  fedha, mipango  na  uchumi  inayoendelea  ya  kutembelea  walengwa  na  kuwapa  elimu  ya  matumizi  sahihi ya ruzuku  wanayoipokea.


Amesema  katika  taarifa  fupi  iliyosomwa  na  mtendaji  wa  kijiji  imebainisha  kuwepo  baadhi  ya  watumishi  wa  serikali ambao  wameajiriwa  kwa  lengo  la  kutoa  huduma  kwa  wananchi  lakini  wanashindwa kufanya  hivyo  wakihitaji  kulipwa  au  kusababisha  mazingira  ya  kupewa  rushwa  hivyo  hawatamvumilia  mtu  huyo.



Mashanda  amewataka  walengwa  wa  mpango  wa  TASAF III  kutumia  ruzuku  wanayoipokea  kwa  malengo  yaliyokusudiwa  na watakaoenda  kinyume  na   malengo  hayo  kwa  kunywa  pombe  na  kufanyia  mambo  ambayo  yanachangia  kurudisha  maendeleo  nyuma  hawatasita  kumwondoa  mara  moja  kwenye  mpango.




Amewataka  pia  kuhakikisha  wanaweka  mkakati  wa  utunzaji  mazingira  kwa  kupanda  miti  rafiki  ya  kutunza  uoto  wa  asili  pia  watumie  fursa  hiyo  kama  njia  ya  kujikwamua  kiuchumi  kwani  wakipanda  miti  ya  matunda  wataweza kuuza  na  kujiingizia fedha.



Naye    diwani  wa  Nyakahanga  Charles  Bechumila  ambaye  ni  mwenyekiti  wa  kamati  ya  kudumu  ya   afya,elimu  na  maji  amewataka  walengwa  wa  mpango  huo  kujiunga  na  mfuko  wa  jamii  wa  CHF  ili  waweze  kupatiwa  matibabu ya  bure  kwa  mwaka  mzima  kwa  Kaya  yenye  watu  sita  wanachangia  shilingi  elfu  kumi  na  Tano  tu.


 Hii ilikuwa  nyumba  ya  mlengwa kijiji kanoni jina  ninalihifadhi


Hata  hivyo  walengwa  waliotembelewa   kwenye  makazi  yao  wameelezea  pesa  hizo  zilivyowasaidia  kubadilisha  maisha  yao na  sasa  walivyo  kutokana  na  kupokea  ruzuku  hiyo.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top