Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: UPUNGUFU WA MADAWATI WAWAKUTANISHA WADAU KITUNTU KARAGWE
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
Wadau   wa   maendeleo   katika   Kata   ya   Kituntu   wilayani Karagwe wamekutana   na   kujadiliana juu   ya   kutatua   Changamoto y...

Wadau  wa  maendeleo  katika  Kata  ya  Kituntu  wilayani Karagwe wamekutana  na  kujadiliana juu  ya  kutatua  Changamoto ya madawati katika shule za msingi kwa kata hiyo.

Hatua  hiyo  imefikiwa  baada  kubaini  upungufu wa zaidi wa  madawati 687 katika kata hiyo kwa shule za msingi, hali ambayo imewalazimu viongozi wa kata  kuitisha wadau wa maendeleo ya upatikanaji wa miti ya kupasua  kupata mbao  za  kutengenezea madawati ili kunusuru tatizo hilo.

Kwenye kikao hicho Afisa Elimu wa kata ya kituntu Sabino Gaudini amesema upungufu wa madawati hayo, umesababaisha watoto kuendelea kukaa chini na wengine kulazimika kubanana kwenye madawati hayo hali ambayo inaweza kusababisha ufahuru mdogo kwa wanafunzi hao.

Kuitishwa kikao cha wadau hao ni kutaka kusaidia kupunguza michango mikubwa kutoka kwa wananchi wa kawaida ,ambapo mbao zaidi ya 1,300 za awali  zinahitajika kutengeneza madawati 250.

Wamesema kuwa kikao cha Kwanza kilichoitishwa kiliwashilikisha wadau kutoka kwenye makanisa, Taasisi za shule na watu binafsi walioweza kuchangia miti 49 na ikiunganishwa na kikao cha leo miti 61 imepatikana tiyari kwa ajili ya upasuaji wa mbao hizo.

Aidha zimetajwa shule ambazo zinaitaji madawati hayo kwa sasa ni Shule ya msingi Kinyinya,Katwe,Maboresho,Katembe ambazo kwa ujumla zimo ndani kata hiyo.

Hata hivyo uongozi wa kata umeomba wanachi kuwa na mwitikio mzuri katika uchangiaji wa madawati ili kutatua swala hilo ambalo litasaidia watoto wao kushiliki vizuri masomo yao kwa ajili ya ufahuru  wa masomo yao.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top