Kutokana na sukari kupanda na kila
mmoja kujipangia bei yake manispaa ya bukoba imeteua mawakala wa maduka
42 ya kuuza sukari kwa wananchi kwa bei elekezi ya serikali ya
shilingi 1800 .
Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari
mkuu wa wilaya ya BUKOBA JAKSONI MSOME amesema mpaka sasa zimeundwa kamati
ndogo ya watendaji ambayo imepangiwa majukumu ili kuhakikisha zoezi linaenda
vizuri.
Ametaja majukumu ya kamati hiyo kuwa
ni kubaini kiasi cha sukari kinacholetwa kutoka kiwandani kwenda kwa
wakala,kutoa mgao wa sukari kwa tasisi maalumu zenye huitaji kama vile mashule
hosipital na vituo vya watoto yatima pamoja na kufuatilia maeneo ya kata kama
bei elekezi ikizingatiwa.
Amebainisha kuwa viongozi na maafisa
watendaji ngazi zote wanajukumu la kusimamia na kuhakikisha wananchi
wanapata huduma bora kwa bei elekezi ya sukari.
Hata hivyo msome amesema kwa
mfanyabiashara ambaye atakiuka maagizo atachukuliwa hatua kali za kisheria.
Zoezi hili la kupanga maduka ya
kuuzia sukari elekezi limekuja baada ya wafanyabiashara kujipangia bei tofauti
na kila mmoja kuuza bei yake kwa kigezo cha sukari kupanda ikiwa kg moja
ilikuwa ikiuzwa shilingi 2200 hadi 2300.
Post a Comment