Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: WAHAMIAJI HARAMU 58 WANASWA MKOANI KAGERA KUINGIA NCHINI KINYUME CHA SHERIA
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
Idara ya uhamiaji mkoani Kagera imewakamata wahamiaji haramu 58 kwa kosa la kuingia nchini kinyume cha sheria  katika kipindi cha siku 13 za...
Idara ya uhamiaji mkoani Kagera imewakamata wahamiaji haramu 58 kwa kosa la kuingia nchini kinyume cha sheria  katika kipindi cha siku 13 za mwezi Juni mwaka huu.

Mkuu wa uhamiaji mkoa wa Kagera, ABDALLAH TOWO amesema  kuwa, kati ya wahamiaji hao, raia wa Burundi ni 42, Rwanda 12, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ni wawili  na Uganda wawili.


Aidha katika hatua nyingine  TOWO amesema kuwa, idara hiyo ipo katika mchakato wa kuwarejesha nchini mwao raia wanne wa Ethiopia  waliomaliza  kifungo chao cha mwaka mmoja, baada ya kuhukumiwa kifungo hicho kutoka na kosa la kuingia nchini kinyume cha sheria.

Hata hivyo amewataka wageni kufuata sheria za nchini huku akiwataka wakazi wa mkoa wa KAGERA kuwaulizia uraia wageni wanapotoka katika nchi zao ili  kuwajua vizuri.


About Author

Advertisement

Post a Comment

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top