Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: WATANZANIA 56 WAUWAWA KATIKA MTO KAGERA MPAKANI MWA TANZANIA NA RWANDA
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
Wananchi   wa   vijiji   vya   Muguruka   na   Chamchuzi   katika   kata   ya   Bweranyange   wilaya   ya   Karagwe   Mkoani  ...





Wananchi  wa  vijiji  vya  Muguruka  na  Chamchuzi  katika  kata  ya  Bweranyange  wilaya  ya  Karagwe  Mkoani  Kagera  wameiomba  serikali  ya  Jamhuri  ya  Muungano  wa  Tanzania  kuimarisha  ulinzi  wa  mpaka  wa  Tanzania  na  nchi  ya  Rwanda  kwenye  mwalo  wa  Rukombe  na  visiwa  vilivyopo  kandokando  ya  mto  Kagera  kutokana  na  kuwepo  vitendo  vingi  vya  uharifu.


Wakizungumza  Jana  katika  mkutano  wa  hadhara  uliofanyika  katika    kijiji  cha  Muguruka    kata  ya  ya  Bweranyange  ulioitishwa  na  mkuu  wa  wilaya  ya  Karagwe  Godfrey  Mheluka  ambao  ulikuwa  na  lengo  la  kuwasikiliza  wananchi  kutoa  maoni  na  ushuhuda  wa  vitendo  vya  uharifu  ambavyo  vimeishapoteza  maisha  ya  Watanzania  wengi.




Godoliva  Gidioni  (43)alisema  tatizo  la  uharifu  wa  wananchi  kupigwa  risasi  hata  kama  wapo  kwenye  shughuli  zao  binafsi  ni  mkubwa  mno  na  yeye  alinusurika  kuwawa    mwaka 2004  ambapo  alikuwa  na  mme  wake  na mtoto   katika  kisiwa  cha  Mubari  kilichopo  mpakani  walivamiwa  na  watu  wanaosadikiwa  ni  askari  wa  doria  kwenye  ziwa  la IHEMA  ambalo lipo  nchi  jirani  ya  Rwanda



“Kweli  kwenye  kisa  hicho  nilikuwa  nimebeba  mtoto  walipiga  risasi  ya  kwanza  ikampata  mme  wangu  Gidion Balembengaro (30) akauwawa  mimi  nilianza  kukimbia  nikiwa  na  mtoto  mgongoni  lakini  nilipatwa  na  risasi  ambayo  ilimpiga  mwanangu  Rehema  Gidion  miezi( 10)   kipindi  hicho  likapitiliza  likanipata  mimi  upande  wa  mkono  wa  kulia  unaona  hii  alama  hivyo  kushtuka  nikakuta  mtoto  wangu  alishafariki”Alisema  Godoliva




Dominick  Benjamini  (41)alisema  jambo  la  ulinzi  kwenye  mwalo  wa  Rukombe  na  visiwa  vya  Mubari,Kisayo,Mto  Kagera  na  Kizinga  ni  muhimu  kuimarishwa  hata  inavyotokea  mtanzania   anaenda  kwenye  maeneo  hayo  wakikutwa  wanapigwa  risasi  tena  mchana   alisema  watu  hao  wanakuwa  na  bodi  na  wanasadikika  kuwa  ni  askari  wanaofanya  doria  kwenye  ziwa  la  akiba  la  IHEMA lililopo  Rwanda.




“Akimwonyesha  mkuu  wa  wilaya  ya  Karagwe  Godfrey  Mheluka  kovu  la  risasi  alilopigwa  kwenye  bega  la  mkono  wa  Kulia  na  kwenye  kiganja  cha  mkono  wa  kushoto  alisema  alipigwa  risasi  hiyo  Agosti 16  mwaka 2013   na  alijiokoa  kwa  kijificha  kwenye  tingatika  lilipo  mpakani  mwa  Tanzania.




Kwa  upande  wake  Agustine   Ngambeki (50)alisema  yeye  alikamatwa  Agosti 03  mwaka  huu  wakati  akiwa  eneo  la  mto  Kagera  alipokuwa  amehaidiana  na  wafanyabiashara  wa  Rwanda  kumuuzia  samaki  kwani  eneo  hilo  ni njia  hivyo  alikutwa  hapo   akanusurika  kupigwa  risasi  baada  ya  mmoja  wa  wanaofanya  doria  kutompiga  risasi  kwani  eneo  hilo  lilikuwa  la  Tanzania.


“Nilisurika  kwasababu  kulikuwepo  watanzania  wengine  wanapita  hivyo  nikatoa  taarifa  kwao na  wao  kuzifikisha  kwenye  uongozi  wa  serikali  ya  kijiji  ambapo  na  wao  walipeleka  taarifa  kwenye  ngazi  ya  wilaya  nilipelekwa  hadi  nchi  Rwanda  nikawekwa  gerezani  lakini  tarehe  10  mwezi  huu  mwenyekiti  wa  kijiji  alifika  nchini  Rwanda  na  kuhaidiwa  wataniachia  na  Agosti 19  mwaka  huu  nilikabidhiwa  kwenye  mpaka  wa  Rusumo  ndiyo  nikalijea  hapa  nashukuru  uongozi  na  wananchi “Alisema  Ngambeki.





Akisoma  taarifa  ya  kata  hiyo  Afisa  Elimu  kata  ya  Bweranyange  Godwin  Mbeikya  kwa  niaba  ya  Mtendaji  wa  Kata  alibainisha  kuwa  tangu  mwaka 1972  watanzania  waliouwawa  kwa  kupigwa  risasi  kwa  vitendo  vya  uharifu  ni  56  ambapo  kijiji  cha  Muguruka  ni 20  na  Chamchuzi  ni  watu 30  na   wajane  ni  21 alibainisha   kuwa  wanaiomba  serikali  ya  Tanzania  kuweka  kivuko  kwa  ajili  ya  kuimarisha  ujirani  mwema.


Alisema kuwa  hao  ni  baadhi  ya  watanzania  waliotoa  taarifa  kwa  serikali  za  vijiji  na  kata  lakini  wapo  wengi  ambao  hawatoi  taarifa  hivyo kuna  uwezekano  wa  idadi  kuongezeka kama  zingelipotiwa  zote.

Mkuu  wa  wilaya  ya  Karagwe  baada  ya  kusikiliza  shuhuda  za  wananchi  hao  amepiga  maruku  mwananchi  yeyote  yule  kuvua  samaki  kwenye  Ziwa  IHEMA  kwani  halipo  nchi  ya  Tanzania  na  kuwataka  kutoendeleza  shuguli  za  uvuvi  kwenye  Mto  Kagera  na kutofanya  shughuli   katika  visiwa  vya  Mubari,Kizinga  na  Kisayo  mpaka  pale  serikali  itakapo  kamilisha  utaratibu  wa  kupata  boti  ya  kuimalisha  ulinzi  katika  mpaka  huo.






Pia  amuagiza  mkuu  wa  polisi  kwa  kushirikiana  na  wanajeshi  wa  jeshi  la  wananchi  wa  kambi  ya  Chamchuzi  na  Kashanda  kufanya  oporesheni  ya kuwaondoa   watu  wote   waliovamia  kwenye  visiwa  vyote  vilivyopo  Tanzania  ambao  inasadikika  siyo  watanzania  na  wanajihusisha  na  ulimaji  Bangi  na  mirungi  na  ameongeza  kuwa  bado  kamati  ya  ulinzi  na  usalama  inakusanya  taarifa  na  baada  ya  kukamilika  zitapelekwa  kwa  waziri  wa  mambo  ya  ndani  kwa  ajili  ya  hatua  zaidi  za  kufanya  mawasiliano  na  serikali  ya  nchi  ya  Rwanda  hivyo  akawataka  wananchi  kuwa  watulivu.






Hata hivyo  Agosti 11 mwaka  huu  waziri  wa  mambo  ya  ndani  wa  Jamhuri  ya  Muungano  wa  Tanzania  Mwigulu  Nchemba  alitembelea  mwalo  wa  Katwe  wilayani  Kyerwa  baada  ya  kuwepo  taarifa  za  watanzania  wawili Emmanueli Kahonda (35) Mkazi  wa Kitwechenkula  wilayani  Kyerwa  na Mfuruki  Felesian (40) mkazi  wa Rubwera   wilaya  ya  Kyerwa    waliuwawa    Agosti  8  mwaka  huu.



Waziri wa mambo ya ndani ya nchini Mwigulu Nchemba aliiagiza kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya ya Kyerwa kukutana na viongozi wa mialo ya Rubwera, Kanyika, Katwe na Ruko  ili wapate taarifa rasmi ya chanzo cha matukio hayo na kuipatia wizara ili waweze kutoa tamko rasmi juu ya mauaji hayo ya wavuvi.





"Hali hii imenistua sana,hatuwezi kuruhusu watanzania wenzetu wawe wanauwawa kikatili kiasi hiki,nikipata taarifa rasmi nitafuatilia jambo hili hata kwa kuwasiliana na wenzetu ili nijue kama ni msimamo wa serekali yao au ni uhalifu"alisema Nchemba.



























About Author

Advertisement

Post a Comment

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top