Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: BREAKINGNEWS ;UKAWA WATANGAZA UAMUZI MGUMU JUU YA BUNGE KUTORUSHWA LIVE.BOFYA HAPA
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
Vyama  vinavyounda  umoja  wa  Katiba  UKAWA wamesema  hawatachangia  bajeti  yoyote  ile  ya  wizara  mpaka  pale  serikali  itakapo...



Vyama  vinavyounda  umoja  wa  Katiba  UKAWA wamesema  hawatachangia  bajeti  yoyote  ile  ya  wizara  mpaka  pale  serikali  itakaporuhusu  kurushwa  moja  kwa  moja  matangazo  hayo (LIVE)uamuzi  huo  umetangazwa  leo  baada  ya  utaratibu  uliokuwepo  zamani ya  kila  mwandishi  kuingia  Bungeni  akiwa  na  vifaa  vyake  vya  kazi  na  kurekodi  matukio  muhimu  anayoona  ni  habari  lakini  nao  umefutwa  na  badala  yake  wanapewa  matukio  yaliyorecodiwa  na  uongozi  wa  Bunge  ndiyo  watangaze  hayo.



Awali  serikali  ilisema  shirika  la  utangazaji  Tanzania  halitanguwa  linarusha  moja  kwa  moja  (LIVE)kwani  wanabana  gharama  za  matangazo  lakini  vyombo  binafsi vilikubali  kurusha  kwa  gharama  zao  lakini  awamu  hii  vimebanwa  na  badala  yake  uongozi  wa  Bunge  ulitangaza  mfumo  mpya  kuwa  watakuwa  na  studio  yao  maarufu  ambayo  vyombo  vyote  vitapata  kutokea  hapo.


Mfuko  wa  kufadhili  vyombo  vya  habari na  waandishi  wa  habari(TANZANIA  MEDIA  FOUNDATION(TMF) walisema  wako  tayari  kutoa  pesa  kugharimia  matangazo  hayo  ili   wananchi  waweze  kupata  kufuatilia  kinachoendelea  kwa  chombo  hicho  muhimu  cha  kutunga  sheria  na  cha  wawakilishi  wa  wananchi  hapa  nchini  mpaka  sasa  serikali  haijawahi  kutoa   majibu  juu  ya  ombi  hilo.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top