Jumuia ya
wazazi ya chama
cha Mapinduzi (CCM)imetoa
msaada wa madaftari,kalamu na
sabuni kwa wanafunzi
wanaoishi katika mazingira
magumu wanaosoma katika
shule za msingi
za Lukole na
Karalo ambao wanafanya
vizuri darasa wametoa
zawadi hiyo katika
siku ya kilele cha
wiki ya wazazi
ambayo kwa wilaya
ya Karagwe imefanyika
viwanja vya ccm
kata ya IHANDA.
Zawadi hizo
zimekabidhiwa na mwenyekiti
wa jumuia ya
Wazazi (CCM) wilaya ya KARAGWE
Exsavery Buguzi
ambaye pia ni
diwani wa Kata
ya Nyakakika amesema
kuwa wao kama
wazazi wanatambua watoto
wenye mahitaji hivyo wameamua
kutoa zawadi kwa
wanafunzi 15 kila
shule kwa wale
tu wanaofanya vizuri
darasani lakini hawatakomea
hapo kwani wanatambua
uwepo wa wanafunzi
wengine,pia mabalozi wa CCM katani
Ihanda nao wamepatiwa
zawadi pamoja na
kuwatembelea kwenye makazi
yao lengo ni
kutambua mchango wao
walioutoa kwa kipindi
cha kampeini za
uchaguzi mkuu wa
mwaka jana na
kukisaidia chama hicho
kuibuka na ushindi.
Akihutubia wananchi na
wanacha wa chama hicho Mwenyekiti wa Chama cha
Mapinduzi CCM Wilaya ya
Karagwe Robson Mtafungwa
ambaye alikuwa mgeni rasmi
katika kilele cha
wiki ya wazazi
wilayani Karagwe amesema
wakati wa malumbano
ya kisiasa umeisha
kilichobakia ni kuwaamini
viongozi waliopatikana ili waweze kuwatumikia
kwa kutekeleza wale walichowaahidi wananchi.
Amesema kuwa Rais
Magufuli ameonesha njia
kwa kuwatumikia watanzania bila
kujali itikadi za
vyama vyao kwani
wananchi walimkabidhi mamlaka
kuwatumikia na ndiyo
maana katika falsafa
yake ya kutumbua
majipu anatumbua wanaccm
na wasiyokuwa wanaccm.
Naye katibu
wa jumuia IDD MVANO akitoa maelezo
kwa wanachama na
wananchi amesema katika
kusherekea wiki ya
wazazi wameamua kufanya
shughuli kadhaa kwa
kutembelea mabalozi pia
kutoa zawadi kwa
wanafunzi ambao wanaishi katika
mazingira magumu na
wanafanya vizuri darasani kwa kutambua
umuhimu wa wazazi kwa watoto.
Jumuia ya wazazi
ya chama cha
mapinduzi CCM ni moja
ya jumuia muhimu
zinazounda chama hicho
na huwa na
shughuli za wiki
ya wazazi kila
mwaka na kilele
chake kitaifa mwaka
huu zitafanyika mkoani Morogoro.
Hata hivyo
kivutio kikubwa katika mkutano wa
jumuia ya wazazi
ya CCM uliofanyika kijiji
cha Lukole alikuwa
ni mwenyekiti wa
kijiji Prisca Bosco pamoja
na mwenyekiti wa
kitongoji Bosco Kanyomoza
ambao wote wanatokana
na chama cha
demokrasia na maendeleo CHADEMA walihudhuria mkutano
huo pia hao
ni mme na
mke ambapo mwananke
ni mwenyekiti wa
kijiji na mwanaume ni
mwenyekiti wa kitongoji.
About Author
The part time Blogger love to blog on various categories like Web Development, SEO Guide, Tips and Tricks, Android Stuff, etc including Linux Hacking Tricks and tips. A Blogger Template Designer; designed many popular themes.
Advertisement

Related Posts
- KAGERA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA VYAFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KUENDELEA KUJIIMARISHA KUWALINDA RAIA NA MALI ZAO25 Apr 20180
Na: Sylvester Raphael Vyombo ya Ulinzi na Usalama Mkoani Kagera vyafanya mazoezi ya ...Read more »
- MBIO ZA MWENGE WA UHURU KATIKA WILAYA ZA KARAGWE NA NGARA PIA HITIMISHO WILAYANI BIHARAMULO MKOANI KAGERA16 Apr 20180
Na: Sylvester Raphael Mwenge wa Uhuru waendelea kuchanja mbuga Mkoani Kagera kwa ku...Read more »
- MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MKOANI KAGERA NA KUANZA UZINDUZI WA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI YA ZAIDI YABILIONI 1216 Apr 20180
Na: Sylvester Rapahel Mwenge wa Uhuru umepokelewa leo April 8, 2018 Mkoani Kagera na...Read more »
- TIMU YA WATAALAM WA UJENZI KUTOKA NCHINI CHINA YAKAGUA ENEO LA UJENZI WA CHUO CHA VETA KAGERA ILI KUANZA UJENZI MARA MOJA16 Apr 20180
Na: Sylvester Raphael Serikali ya Watu wa China yatuma timu ya Wataalam wa Usanif...Read more »
- MKOA WA KAGERA WAVUKA LENGO KATIKA UNDIKISHAJI WA WANAFUNZI AWALI NA DARASA LA KWANZA MWAKA 201816 Apr 20180
Na: Sylvester Raphael Mkoa wa Kagera wavuka lengo la uandikishaji wa Wananfunzi katika madarasa...Read more »
- MKUU WA MKOA KAGERA AAGIZA MKANDARASI KUKAMATWA NA KUFIKISHWA OFISINI KWAKE AKIWA NA PINGU MIKONONI BAADA YA KUITIA SERIKALI HASARA08 Mar 20180
Na Sylvester Raphael Mkuu wa Mkoa wa Kagera aagiza Mkandarasi wa Kampun...Read more »
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.