What's New?

1:57 PM ADC Summit 2025!

Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: KUFUATIA WIZI WA MIFUGO WANANCHI WATAKIWA KUHAKIKISHA USALAMA WAO NA MALI ZAO
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
Wananchi wameaswa kuhakikisha usalama wa mali zao na watu wengine na kutoa taarifa pale waonapo mali wasizofahamu mmiliki wake ka...




Wananchi wameaswa kuhakikisha usalama wa mali zao na watu wengine na kutoa taarifa pale waonapo mali wasizofahamu mmiliki wake katika vyombo husika vya sheria.

Kauli hiyo imetolewa na mwenyekiti wa Kitongoji Nyakashambya Kijiji cha Nyabwegira Kata ya Ngama Wilayani Karagwe  Laiton John Mlaki  wakati akiongea na chombo hiki baada ya wananchi katika kitongoji chake kuokota Ng’ombe wawili mali ya Anthony Elias Kahigwa mkazi wa Chanika.

Aidha ameushukuru  mtandao huu kwa uharaka wake katika kuhakikisha matangazo ya muhimu yanapewa kipaumbele ili kusaidi wahusika kufanikisha mahitaji yao.

Kwa upande wake Anthony Elias Kahigwa ambaye alipotelewa na Ng’ombe wake hao ameelezea pia umuhimu wa Redio na jinsi alivyopata mafanikio katika matukio tofauti aliyoyapata na kutumia Redio.

Pia amewaasa wananchi wengine kuiga mfano wa wananchi waliotoa taarifa za kupatikana kwa Ng’ombe wake kwa kuzingatia kuwa ni hatua ya uaminifu na usalama katika jamii.


Ng’ombe hawa wamepotea jana majira ya asubuhi na kupatikana majira ya mchana baada ya kukamatwa na wasamalia wema wakiwa wanalanda landa bila kuwa na mchungaji.


Kumekuwa na matukio ya kuibiwa  na kupotea Ng’ombe katika Wilaya ya Karagwe  ambapo wengine wamekuwa wakipatikana huku wengine kutopatikana.
07 Apr 2016

About Author

Advertisement

Post a Comment

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top