Wananchi wameaswa
kuhakikisha usalama wa mali zao na watu wengine na kutoa taarifa pale waonapo
mali wasizofahamu mmiliki wake katika vyombo husika vya sheria.
Kauli hiyo imetolewa na
mwenyekiti wa Kitongoji Nyakashambya Kijiji cha Nyabwegira Kata ya Ngama
Wilayani Karagwe Laiton John Mlaki wakati akiongea na chombo hiki baada ya
wananchi katika kitongoji chake kuokota Ng’ombe wawili mali ya Anthony Elias
Kahigwa mkazi wa Chanika.
Aidha ameushukuru mtandao huu kwa uharaka wake katika
kuhakikisha matangazo ya muhimu yanapewa kipaumbele ili kusaidi wahusika
kufanikisha mahitaji yao.
Kwa upande wake Anthony
Elias Kahigwa ambaye alipotelewa na Ng’ombe wake hao ameelezea pia umuhimu wa
Redio na jinsi alivyopata mafanikio katika matukio tofauti aliyoyapata na
kutumia Redio.
Pia amewaasa wananchi
wengine kuiga mfano wa wananchi waliotoa taarifa za kupatikana kwa Ng’ombe wake
kwa kuzingatia kuwa ni hatua ya uaminifu na usalama katika jamii.
Ng’ombe hawa wamepotea jana
majira ya asubuhi na kupatikana majira ya mchana baada ya kukamatwa na wasamalia
wema wakiwa wanalanda landa bila kuwa na mchungaji.
Kumekuwa na matukio ya
kuibiwa na kupotea Ng’ombe katika Wilaya
ya Karagwe ambapo wengine wamekuwa
wakipatikana huku wengine kutopatikana.
About Author
The part time Blogger love to blog on various categories like Web Development, SEO Guide, Tips and Tricks, Android Stuff, etc including Linux Hacking Tricks and tips. A Blogger Template Designer; designed many popular themes.
Advertisement

Related Posts
- KAGERA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA VYAFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KUENDELEA KUJIIMARISHA KUWALINDA RAIA NA MALI ZAO25 Apr 20180
Na: Sylvester Raphael Vyombo ya Ulinzi na Usalama Mkoani Kagera vyafanya mazoezi ya ...Read more »
- MBIO ZA MWENGE WA UHURU KATIKA WILAYA ZA KARAGWE NA NGARA PIA HITIMISHO WILAYANI BIHARAMULO MKOANI KAGERA16 Apr 20180
Na: Sylvester Raphael Mwenge wa Uhuru waendelea kuchanja mbuga Mkoani Kagera kwa ku...Read more »
- MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MKOANI KAGERA NA KUANZA UZINDUZI WA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI YA ZAIDI YABILIONI 1216 Apr 20180
Na: Sylvester Rapahel Mwenge wa Uhuru umepokelewa leo April 8, 2018 Mkoani Kagera na...Read more »
- TIMU YA WATAALAM WA UJENZI KUTOKA NCHINI CHINA YAKAGUA ENEO LA UJENZI WA CHUO CHA VETA KAGERA ILI KUANZA UJENZI MARA MOJA16 Apr 20180
Na: Sylvester Raphael Serikali ya Watu wa China yatuma timu ya Wataalam wa Usanif...Read more »
- MKOA WA KAGERA WAVUKA LENGO KATIKA UNDIKISHAJI WA WANAFUNZI AWALI NA DARASA LA KWANZA MWAKA 201816 Apr 20180
Na: Sylvester Raphael Mkoa wa Kagera wavuka lengo la uandikishaji wa Wananfunzi katika madarasa...Read more »
- MKUU WA MKOA KAGERA AAGIZA MKANDARASI KUKAMATWA NA KUFIKISHWA OFISINI KWAKE AKIWA NA PINGU MIKONONI BAADA YA KUITIA SERIKALI HASARA08 Mar 20180
Na Sylvester Raphael Mkuu wa Mkoa wa Kagera aagiza Mkandarasi wa Kampun...Read more »
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.