Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: KAGERA NAO WAENDELEA NA ZOEZI LA KUHAKIKI SILAHA ZAO KUTII AGIZO LA JESHI LA POLISI
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
Jeshi la polisi mkoani KAGERA limewaagiza wananchi wote  na makampuni binafsi wanaomiliki silaha bila kufuata taratibu na sheria...




Jeshi la polisi mkoani KAGERA limewaagiza wananchi wote  na makampuni binafsi wanaomiliki silaha bila kufuata taratibu na sheria kusalimisha silaha zao katika kituo cha polisi au ofisi za vijiji na mitaa.

Akizungumza na waandishi wa habari wa  kamanda wa jeshi la polisi mkoani KAGERA AGUSTINI OLLOMI amesema kuwa zoezi hili linawahusu wananchi wote wanaomiliki silaha pamoja na makampuni binafsi yanayomiliki kinyume na sheria.
 
Amefafanua kuwa  zoezi hili limetangazwa na serikali hivyo wananchi wote wanaomiliki silaha kinyume na sheria inabidi wazisalimishe hivyo ametumia kuwaomba wananchi wasalimishe silaha hizo kwa hiari yao wenyewe kabla hatua kali za kisheria hazijachukuliwa.


Aidha amewataka wale wote ambao ndugu zao wametangulia mbele ya haki kama wameacha silaha kutafuta mirathi  yao ili kuzipeleka  silaha hizo katika kituo cha polisi ili zitambuliwe.



Hata hivyo OLLOMI amewataka wananchi kuwafichua wale wote ambao wanamiliki silaha ambao hawatakuwa tayari kusarimisha silaha zao kwa hiari katika vijiji na mitaa au kituo cha polisi ili wachukuliwe hatua kali za kisheria.

Zoezi la kuhakiki silaha mkoani KAGERA litaanza rasmi April MOJA hadi Juni 30  mwaka huu lengo ikiwa ni kujua idadi ya wananchi wanaomiliki silaha mkoani KAGERA.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top