Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: WAZEE WAIOMBA SERIKALI KUFUATILIA SERA YA MATIBABU BURE ILI KUWASAIDIA KUPATA HUDUMA
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
Wazee Wilayani Karagwe wameiomba serikali kufuatilia utekelezaji wa sera ya matibabu bure kwa wazee katika baadhi ya vituo vya Af...




Wazee Wilayani Karagwe wameiomba serikali kufuatilia utekelezaji wa sera ya matibabu bure kwa wazee katika baadhi ya vituo vya Afya na zahati Hapa nchini ili kuwawezesha kupata huduma ya Afya inayostahili.


Wakizungumza na KARAGWE FORUM  baadhi ya wazee wa kijiji cha Rwambaizi  kata ya Kanoni hapa wilayani Karagwe wamesema kuwa pamoja na sera kutamka kuwa wazee wapate huduma ya matibabu bure lakini bado wanatumia gharama zao kupata matibabu katika vituo vya Afya na Zahanati nap engine kuagizwa sehemu ya kwenda kununua dawa.

Mzee Venant Dio Rukehata mwenye Umri wa miaka 81 ameelekeza kilio chake kwa Wizara ya Afya  maendeleo ya jamii jinsia, wazee na watoto kuhakikisha wazee wanapata matibabu bure kama  sera inavyoelekeza.

Kwa upande wake Bertha Sospeter  amesema wazee hawathaminiwi pale wanapokwenda katika vituo vinavyotoa huduma ya matibabu hali inayowakatisha tamaa na kuitaka serikali kutambua kuwa wazee wananchango mkubwa katika maendeleo ya Nchi.

Naye mzee Dionizi Kyaruzi Rwabwigamo ameimba serikali kujenga vituo vya Afya na zahanati za serikali katika kijiji chao hili kusogeza huduma ya Afya karibu ambapo itawaepushia ghama wanazotumia kufuata matibabu katika umbali mrefu.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Rwambaizi Gosbert Paulo Katabarwa amekiri kuwepo changamoto ya ukosefu wa Zahanati na Kituo cha Afya katika kijiji hicho na kuwa hali hiyo inasababisha wazee wengi katika kijiji hicho kupata matibabu kwa shida japo hana idadi sahihi ya wazee walio katika kijiji chake.

Aidha amesema katika kukabiliana na changamoto wanazokutana nazo wazee katika kupata huduma ya matibabu kijiji kina mpango wa kujenga Zahanati ili wananchi na wazee waweze kupata huduma hiyo karibu

About Author

Advertisement

Post a Comment

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top