What's New?

1:57 PM ADC Summit 2025!

Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: KILIO CHA MUDA MREFU CHA WATU WENYE UALIBINO MKOA WA KAGERA CHAANZA KUTATULIWA
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
Kufuatia kilio cha muda mrefu kwa watu wenye ualbino kuhitaji kupatiwa huduma ya matibabu bure bila mafanikio   shirika lisilokuwa...



Kufuatia kilio cha muda mrefu kwa watu wenye ualbino kuhitaji kupatiwa huduma ya matibabu bure bila mafanikio  shirika lisilokuwa la kiserikali la Standing Voice lenye makao yake Mkoani Mwanza limejitolea kuwasaidia mafuta ya Ngozi na ukaguzi wa Afya ya Kansa ya Ngozi katika Baadhi ya Vituo vya Afya  vya Kanda ya Ziwa.

Hayo yamethibitishwa na Katibu wa chama cha watu wenye Ualbino Mkoa wa Kagera Ignas Lugemalira na kubainisha vituo vya Afya vitakavyotoa huduma hiyo kwa Mkoa wa Kagera pamoja nawilaya zitakazohusika.

Lugemalira amekieleza chombo hiki kuwa hatua hii imekuja baada ya kuangaika kwa muda mrefu bila kupata matokeo chanya juu ya hatma ya Afya ya watu wenye ualbino.

Aidha ameeleza kusikitishwa na ahadi za serikali zisizotekelezeka na kwamba bado watu wenye ualbino hawajapewa kipaumbele katika nchi yao kama yalivyo makundi mengine.

Amesema zoezi hili ni mwendelezo huku akitaja kukabiliwa na changamoto ya mahudhurio hafifu ya watu wenye ualbino kutokana na Halmashauri za wilaya husika kushindwa kuwasafirisha kwenda kupata huduma katika vituo vilivyotajwa.

Lugemalira ameiomba jamii pamoja na serikali ya Tanzania kutoa ushirikiano kwa watu wenye Ualbino kuhakikisha wanafikiwa huduma kama zinavyokuwa zikitolewa kwani wanastahili kupata haki zao za msingi kama yalivyomakundi mengine.
07 Apr 2016

About Author

Advertisement

Post a Comment

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top