Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: MWENGE WA UHURU KUZINDUA NA KUWEKA MAWE YA MSINGI MIRADI YA MILLIONI 911,695,000 KARAGWE
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
Jumla ya miradi kumi ya maendeleo ya wilayani Karagwe mkoani Kagera yenye thamani ya shilling   milioni   911,695,000 e inatara...





Jumla ya miradi kumi ya maendeleo ya wilayani Karagwe mkoani Kagera yenye thamani ya shilling  milioni  911,695,000 e inatarajiwa kuzinduliwa na kuwekea jiwe la msingi wakati wa mbio za  mwenge wa uhuru ambao utapokelewa wilayani Karagwe tarehe 26 mwezi wa 7 mwaka  huu



Hayo yamesemwa leo na mratibu wa mbio za mwenge wilaya  ya  Karagwe Aloyce Mjungu wakati akiongea na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya mbio za mwenge ambayo yanaendelea katika wilaya hii.



Mjungu amesema kuwa mwenge wa uhuru utapokelewa tarehe 26 mwezi wa saba mwaka huu katika shule ya msingi Muungano katani Nyakasimbi na ndiko utaanzia kutembelea miradi ya maendeleo ambapo utaweka jiwe la msingi katika nyumba ya walimu yenye vyumba sita shule ya Sekondari Nyakasimbi yenye Thamani ya shilingi milioni 150.


Ametaja miradi mingine kuwa ni uzinduzi wa club ya wapinga Rushwa katika shule ya sekondari Rugu,uzinduzi wa shamba la miti Kasheshe Rugu pamoja na miradi mingine kama anavyoeleza.



 Ameongeza kuwa baada ya uzinduzi wa miradi hiyo yote mwenge utakesha katika viwanja vya Changarawe mji mdogo wa Kayanga na wataukabidhi wilayani Kyerwa tarehe 27 mwezi wa saba mwaka huu katika shule ya msingi Ilega iliyoko katika kata ya Mabira wilayani Kyerwa.



Mjungu amewataka wananchi kuchangia mwenge wa uhuru kwani unakuja kwa ajili ya wananchi wote bila kujali kabila,rangi au itikadi. 


About Author

Advertisement

Post a Comment

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top