Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: WAHIMIZWA KUFUATA SHERIA,TARATIBU NA KANUNI KATIKA KUISHI NA JAMII
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
Wananchi wanaomiliki Ardhi wametakiwa kufuata kanuni, sheria na taratibu hasa katika kuziba na kuanzisha barabara ambazo zinapita katika...

Wananchi wanaomiliki Ardhi wametakiwa kufuata kanuni, sheria na taratibu hasa katika kuziba na kuanzisha barabara ambazo zinapita katika maeneo yao.

Wamesema hayo wananchi wa Mtaa wa Rwenjonjo eneo la Ahakakoma Kata ya Ihanda  katika mkutano wa pamoja kufuatia kutaka kuzibwa kwa moja ya barabara iliyoko mkabala na uwanja wa Ndege Ihanda kuelekea Kigasha.

Katika mkutano huo umehudhuriwa na wananchi wa maeneo husika, viongozi mbali mbali akiwemo mwenyekiti wa mtaa huo, Diwani wa Kata ya Ihanda na Afisa mtendaji wa Kata hiyo kwa agizo la Mkuu wa Wilaya ya Karagwe kumaliza mgogoro wa moja ya barabara katika maeneo hayo kutaka kuzibwa na moja ya familia ambao walipeleka mashtaka katika ofisi ya mkuu wa Wilaya kuwa barabara hiyo imeanzishwa katika ardhi ya mtoto yatima.


Wanaolalamikia kuwepo kwa barabara hiyo hiyo ni Aquilina Revelian na Eusebia Reveliana wanaodai kuwepo na barabara tatu katika ardhi yao hivyo kutaka kuziba moja ya barabara hizo kwa lengo la kuokoa ardhi ya mtoto yatima wanayemlea kwani ni eneo lake na kusema kuwa wanaotaka kuendeleza barabara hiyo wanapaswa kukaa pamoja nao kwa ajili ya makubaliano na kupewa fidia na si vinginevyo.


Aliyelalamikiwa na familia hiyo kwa kuanzisha barabara hiyo ni  Odilo Binemungu ambaye amesema kuwa yeye hakwenda kuanzisha barabara mpya katika eneo linalodaiwa bali alitimiza jukumu lake la kujitolea katika barabara hiyo kama ilivyo kawaida ya wananchi wa eneo hilo na kusema kuwa barabara hiyo ameikuta tangu amezaliwa na hana budi kuiendeleza.


Wazee wa eneo hilo walizaliwa kuanzia miaka ya 1930 wameeleza kuwa barabara hiyo ni ya tangu zamani na watu wa kuelekea Kigasha walikuwa wanaitumia katika shughuli za maendeleo na haijaanzishwa leo wala jana kama wafungua mashtaka wanavyosema.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top