Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: WASIWASI WA UHABA WA MVUA KARAGWE WANANCHI WATAKIWA KULIMA MAZAO YA KINGA
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
Afisa mtendaji wa kata ya Nyakasimbi wilayani Karagwe mkoani Kagera Medard Baletwa amewaagiza viongozi wa vitongoji na vijiji kuhakikish...

Afisa mtendaji wa kata ya Nyakasimbi wilayani Karagwe mkoani Kagera Medard Baletwa amewaagiza viongozi wa vitongoji na vijiji kuhakikisha wanasimamia zoezi la kilimo cha Kinga ya njaa kwa kila familia.

 Baletwa amesema kuwa  ni bora wakulima wakatumia mvua hizi zinazoendelea kunyesha kupanda mazao ya kinga ya njaa hususani yale yanayokomaa kwa muda mfupi.

Amesema kuwa ni jukumu la kila kiongozi wa kitongoji na kijiji pia kuhakikisha anasimamia kila familia inapanda mazao hayo ambayo ameyataja kuwa ni mihogo,malando, viazi na magimbi  ambapo kila familia itatakiwa kupanda hekali kadhaa kama watakavyokuwa wameelekezwa.


Amesema kuwa kufuatia agizo la mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Karagwe Wailles Mashanda la afisa watendaji kusimamia kilimo cha kinga ya njaa,Baletwa amesema atazungikia kata nzimakwa kushirikiana na viongozi wa vijiji ili kuhimiza kilimo hicho pamoja na shuguli nyingine za maendeleo.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top