Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: WAKRISTO WATAKIWA KUWA NA HAMU YA KUTUMIA MUDA WAO MWINGI KUWA NA YESU KRISTO
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
Wakristu wametakiwa kuwa na hamu ya kumpokea bwana Yesu Kristu katika kumtumikia na kugawana muda wake pamoja naye.  Wito huo umetol...

Wakristu wametakiwa kuwa na hamu ya kumpokea bwana Yesu Kristu katika kumtumikia na kugawana muda wake pamoja naye. 

Wito huo umetolewa leo na Baba Askofu wa Jimbo Katoliki la Kayanga  Askofu Almachius Vicent Rweyongeza katika Ibada takatifu ya sherehe ya mwili na damu ya Yesu Kristu yaani Ekaristi takatifu.

Katika Ibada hiyo hiyo ya Ekaristi takatifu Askofu Almachius amesema wakiristu wanapaswa kuwa na hamu ya kumpokea na kugawana muda wao pamoja naye.

Rweyongeza amesema katika kumpokea Watu wasingangania dhambi hasa kwenye familia ambayo ni kutopata sekramenti ambayo husababisha ndoa za mitara na kuvunja amri ya sita ya Mungu na nyinginezo.

Amesema dhambi hizo ambazo watu wengi huzitenda zimekuwa ni mambo ambayo ni magonjwa ya kiroho yanayoziba wokovu na uzima wa milele na kusababisha mtu kutoendelea katika maisha yake.

Askofu Rweyongeza amesema tiba ya milele katika kufanikiwa ni kujongea sakramenti ya kitubio ili kuondolewa dhambi na kuweza kupata tija ya kiroho ya Kudumu kwa kumpokea yesu kristu ambaye ni Ekaristi takatifu.

Katika sherehe hiyo kumehusishwa misa takatifu, Maandamano ambayo ni kumshudia kiristu bila aibu kutoka kwa watu kwani anakuwa kwani anayefanya hivyo anakuwa amekiri adharani mbele ya watu wengine  kwamba yeye anamtumikia yesu kristu.

Rweyongeza amesema njia ya maandamano imepambwa na nyimbo za sifa za kusifu Ekaristi na maua ambayo ni mwaliko kwa kila mmoja kumpamba yesu kwa kupamba njia ambayo anapita kwa kutumia upendo, utii, uaminifu, mienendo mizuri ambayo itamfanya mkiristu naye kuvutia katika maisha yake.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top