WALENGWA WA TASAF WAOMBA KUONGEZEWA KIWANGO CHA RUZUKU WANAYOPATA
Rai hiyo,imetolewa na walengwa hao kwa nyakati tofauti wakati wa ziara ya Katibu tawala wa Mkoa wa Kagera AMATUS MSOLE wakati amewatembelea walengwa wa mpango huo ili kujionea maendeleo ya miradi yao walioanzisha kutokana na ruzuku wanayopokea kwa kila mwezi.
Devotha Fella mkazi wa mtaa wa Rubumba,pamoja na shukrani kwa serikali juu ya utekelezaji wa mpango huo,ameiomba Serikali kupitia mfuko huo,kufikiria ni jinsi gani inaweza kuongeza kiwango cha ruzuku kutoka 20,000 inayotolewa kwa ajili ya kujikimu,kutokana na gharama za uendeshaji wa maisha kupanda na kusababisha uwepo ugumu wa maisha.
Amesema kuwa kiwango hicho kitaongezeka,kuna uwezekano mkubwa wa kuwepo mabadiriko makubwa baina ya walengwa kutoka kwenye hali ya umasikini kufikia hali ya kawaida ya maisha ya kati kwani mbali na kiwango kinachotolewa kwa sasa kuwa kidogo lakini kimewezesha kusaidia kuwepo kwa mabadiriko ya maisha kwa walengwa. .
Kwa upande wao Stella Pius na Rehema Ismail wote wakazi wa mtaa Rumumba,pamoja na pendekezo hilo la kuongezeka kiwango cha ruzuku,pia wamebainisha kuwa ruzuku itolewayo kwa malengo ya kupambana na umasikini,imewainua sana na kuyafanya maisha yao yaonekane kama rahisi tofauti na hali ilivyokuwa kabla ya kupokea ruzuku.
Akitoa taarifa za mpango huo,Mratibu wa Tasaf III Manispaa ya Bukoba MURISHIDI ISSA,jumla ya shilingi milioni 153,256,500 zimetolewa na mfuko wa maendeleo ya jamii(Tasaf) kwa ajili ya malipo ya ruzuku kwa walengwa 3,876, kiasi cha fedha kilicholipwa wakati wa dirisha la awamu ya sita ya miezi Mei na Juni.
MURISHIDI amesema kuwa kati ya fedha hizo kiasi cha milioni 136,228,000 zilienda moja kwa moja kwa ajili ya ruzuku kwa walengwa,huku kiasi cha 17,028,500 ikiwa ni asilimia 1.5 inayopelekwa kwenye mitaa ili kuwezesha shughuli mbalimbali zikiwemo za ufuatiliaji na usimamizi wa mpango huo.
Kwa upande wake Katibu Tawala mkoa wa KAGERA AMATUS MSOLE amesema mbali na kutoa pongezi kwa baadhi ya walengwa hao walioonekana kufanya mabadiriko kwa kutumia vizuri ruzuku hiyo ya Tasaf,pia ametoa rai kwa walengwa wengine walioko kwenye mfuko kuiga mfano kwa walengwa waliofanikiwa kwa matumizi bora ya fedha za ruzuku.
Hata hivyo MSOLE amesema kuwa nia ya Serikali ni kuondoa watu kwenye umasikini,hivyo baada ya miaka mitatu Serikali haitaendelea kumpatia ruzuku masikini yeyote atakayekuwa tayari ameishapokea ruzuku kwa awamu hii,badala yake utaratibu utakaokuwepo ni kubaini kaya nyingine zilizo masikini na kuziingiza kwenye mpango.
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.