Wananchi na wadau wa
maendeleo wilayani Karagwe mkoani Kagera wamepongezwa kwa jitihada zao za
makusudi waliozoonesha katika kuchangia suala zima la madawati, ambapo hadi
sasa kata zote za wilaya ya Karagwe zimefikisha madawati 2,324 huku halmashauri
ikiwa imeshatoa madawati 500.
Pongezi hizo zimetolewa leo na mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya
Karagwe mkoani Kagera Wailess Mashanda wakati akiongea na KARAGWE FORUM ofisini
kwake.
Mashanda amesema kuwa
wananchi na wadau wa maendeleo wilayani humu wameoonesha jitihada kubwa za
kuchangia madawati japo kufikia juni 30 mwaka huu kama agizo la Rais kuwa
wamekamilisha madawati, kwa wilaya ya Karagwe watakuwa hawajakamilisha japokuwa
wapo katika harakati za kukamilisha baada ya hapo.
Ameongeza kuwa hadi sasa
zoezi la ukusanyaji wa mbao na boriti linaendelea huku waliotoa ahadi za
kuchangia madawati nao wakiwa wanaendelea kutoa michango yao ili kuhakikisha
shule zote za wilaya ya Karagwe zinapata
madawati ya kutosha.
Hata hivyo Mashanda
amewataka wananchi ambao bado hawajachangia mchango huo wa madawati kuhakikisha
wanachangia na kufikia malengo walioyojiwekea katika vijiji,vitongoji na kata
kwa ujumla.
Katika hatua nyingine Mashanda
amezungumzia kuteuliwa kwa mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Karagwe
Mhandisi Richard Ruyango kuwa mkuu wa wilaya ya Muleba na kuhamishwa
kwa mkuu wa wilaya ya Karagwe Deodatus Lucas Kinawiro kuwa mkuu wa wilaya ya
Bukoba.
About Author
The part time Blogger love to blog on various categories like Web Development, SEO Guide, Tips and Tricks, Android Stuff, etc including Linux Hacking Tricks and tips. A Blogger Template Designer; designed many popular themes.
Advertisement

Related Posts
- KAGERA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA VYAFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KUENDELEA KUJIIMARISHA KUWALINDA RAIA NA MALI ZAO25 Apr 20180
Na: Sylvester Raphael Vyombo ya Ulinzi na Usalama Mkoani Kagera vyafanya mazoezi ya ...Read more »
- MBIO ZA MWENGE WA UHURU KATIKA WILAYA ZA KARAGWE NA NGARA PIA HITIMISHO WILAYANI BIHARAMULO MKOANI KAGERA16 Apr 20180
Na: Sylvester Raphael Mwenge wa Uhuru waendelea kuchanja mbuga Mkoani Kagera kwa ku...Read more »
- MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MKOANI KAGERA NA KUANZA UZINDUZI WA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI YA ZAIDI YABILIONI 1216 Apr 20180
Na: Sylvester Rapahel Mwenge wa Uhuru umepokelewa leo April 8, 2018 Mkoani Kagera na...Read more »
- TIMU YA WATAALAM WA UJENZI KUTOKA NCHINI CHINA YAKAGUA ENEO LA UJENZI WA CHUO CHA VETA KAGERA ILI KUANZA UJENZI MARA MOJA16 Apr 20180
Na: Sylvester Raphael Serikali ya Watu wa China yatuma timu ya Wataalam wa Usanif...Read more »
- MKOA WA KAGERA WAVUKA LENGO KATIKA UNDIKISHAJI WA WANAFUNZI AWALI NA DARASA LA KWANZA MWAKA 201816 Apr 20180
Na: Sylvester Raphael Mkoa wa Kagera wavuka lengo la uandikishaji wa Wananfunzi katika madarasa...Read more »
- MKUU WA MKOA KAGERA AAGIZA MKANDARASI KUKAMATWA NA KUFIKISHWA OFISINI KWAKE AKIWA NA PINGU MIKONONI BAADA YA KUITIA SERIKALI HASARA08 Mar 20180
Na Sylvester Raphael Mkuu wa Mkoa wa Kagera aagiza Mkandarasi wa Kampun...Read more »
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.