Mbunge wa Jimbo la Kigamboni (CCM)
Dkt Faustine Ndugulile ameyataka Mataifa kushirikisha Mabunge katika
kufanikisha mpango wa Usalama wa Afya Duniani (Global Health Security Agenda).
Akizungumza kwenye mkutano wa
masuala ya Usalama wa Afya ulioandaliwa na Shirika la Afya Duniani (WHO) na kufanyika
Jijini Bali, Indonesia, ulioanza Juni 27 na kuhitimishwa Juni 30 Dkt Ndugulile amesema, Mabunge yanaweza kutoa
mchango mkubwa sana kwenye utekelezaji wa Mpango wa Usalama wa Afya Duniani kwa
kusimamia Serikali na kuhakikisha hatua zote muhimu zinatekelezwa, kutunga
Sheria zitakazosimamia utekelezaji wa mpango huu pamoja na kuhakikisha mpango
huu unapata fedha za kutosha kutoka kwenye Bajeti ya Serikali.
Aidha Dkt Ndugulile amesema kuwa
muingiliano wa shughuli za kilimo, mifugo na shughuli nyingine za kibinadamu
zimesababisha baadhi ya magonjwa ya wanyama kuleta athari kwa binadamu na pia
usugu wa madawa ya aina ya antibiotiki na kuongeza kuwa kuna haja ya wadau wa sekta hizi kuwa na
ushirikiano wa karibu chini ya mpango wa “Afya Moja”
Amesema kuwa Ili mpango wa “Afya
Moja” ufanikiwe in lazima maboresho yafanyike kwenye uratibu wa sekta
mbalimbali ndani ya nchi na pia kuandaa mpango wa pamoja wa udhibiti na
kushughulikia majanga.
Dkt Ndugulile mbali ya kuwa Mbunge
wa Jimbo la Kigamboni, ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ushauri ya Mabunge Duniani
(Inter Parliamentary Union) kuhusiana na masuala ya UKIMWI, Afya ya Wanawake,
Vijana na Watoto.
About Author
The part time Blogger love to blog on various categories like Web Development, SEO Guide, Tips and Tricks, Android Stuff, etc including Linux Hacking Tricks and tips. A Blogger Template Designer; designed many popular themes.
Advertisement

Related Posts
- KAGERA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA VYAFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KUENDELEA KUJIIMARISHA KUWALINDA RAIA NA MALI ZAO25 Apr 20180
Na: Sylvester Raphael Vyombo ya Ulinzi na Usalama Mkoani Kagera vyafanya mazoezi ya ...Read more »
- MBIO ZA MWENGE WA UHURU KATIKA WILAYA ZA KARAGWE NA NGARA PIA HITIMISHO WILAYANI BIHARAMULO MKOANI KAGERA16 Apr 20180
Na: Sylvester Raphael Mwenge wa Uhuru waendelea kuchanja mbuga Mkoani Kagera kwa ku...Read more »
- MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MKOANI KAGERA NA KUANZA UZINDUZI WA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI YA ZAIDI YABILIONI 1216 Apr 20180
Na: Sylvester Rapahel Mwenge wa Uhuru umepokelewa leo April 8, 2018 Mkoani Kagera na...Read more »
- TIMU YA WATAALAM WA UJENZI KUTOKA NCHINI CHINA YAKAGUA ENEO LA UJENZI WA CHUO CHA VETA KAGERA ILI KUANZA UJENZI MARA MOJA16 Apr 20180
Na: Sylvester Raphael Serikali ya Watu wa China yatuma timu ya Wataalam wa Usanif...Read more »
- MKOA WA KAGERA WAVUKA LENGO KATIKA UNDIKISHAJI WA WANAFUNZI AWALI NA DARASA LA KWANZA MWAKA 201816 Apr 20180
Na: Sylvester Raphael Mkoa wa Kagera wavuka lengo la uandikishaji wa Wananfunzi katika madarasa...Read more »
- MKUU WA MKOA KAGERA AAGIZA MKANDARASI KUKAMATWA NA KUFIKISHWA OFISINI KWAKE AKIWA NA PINGU MIKONONI BAADA YA KUITIA SERIKALI HASARA08 Mar 20180
Na Sylvester Raphael Mkuu wa Mkoa wa Kagera aagiza Mkandarasi wa Kampun...Read more »
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.