Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: WATAKIWA KUFUATA MASHARTI YA KUONGEZA UBORA WA KAHAWA ILI KUPATA BEI NZURI
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
Watendaji   wa   vijiji   na   Kata   wametakiwa   kuzungukia   maeneo   ambayo   wanafanyia   kazi   ili   kubaini   baadhi   ya   waku...

Watendaji  wa  vijiji  na  Kata  wametakiwa  kuzungukia  maeneo  ambayo  wanafanyia  kazi  ili  kubaini  baadhi  ya  wakulima  wa  Kahawa  wanaokiuka  agizo  la  serikali  la  kutovuna  kahawa  mbichi  na  kuzianika  chini  waweze  kuchukuliwa  hatua  za  kisheria  dhidi  yao.


Agizo  hilo  likmetolewa  na  mwenyekiti  wa  halmashauri  ya  wilaya  ya  Karagwe Wallesi  Mashanda  baada  ya  kukuta  mkulima  wa  kahawa  Filidolini  Nestory  wa  kitongoji  cha Omukilama   kijiji  cha  Kanoni  kata  ya  Kanoni  wilaya  ya  Karagwe  amevuna  kahawa  mbichi  kitendo  ambacho  kimeelezwa  ni  kuikosea  Jamhuri  na  baadhi  ya  wakulima  wanaofuata  masharti yaliyowekwa  na  serikali.

Amesema  kutokana  na  hali  hiyo  kujitokeza  watakuwa  wanafanya  ziara  za  kushtukiza  ili  kuwabaini wanaovuna   kahawa  mbichi  na  kuwachukulia  hatua  kali  dhidi  yao .


Kufuatia  hali  hiyo  Walles  Mashanda  ametoa  agizo  kwa  mtendaji  wa  kijiji  cha  Kanoni  Peter  Rwabishengo  kuwatafuta  wanamgambo  kuhakikisha  kahawa  hizo  mbichi  zinazolewa  na  kuteketezwa  ambapo  wanangambo  watatu  Agustine  Elias,Majaliwa  Edward  na  Philimoni  Rugarabamu  wakaanza  kutekeleza  agizo  hilo.
Hata  hivyp  mkulima  Revelian  Kamuhangile   ambaye  amekutwa  akianika  kahawa  zao  amepongezwa  na  kamati  hiyo  kwa  kuanika  kahawa  vizuri  na  zilizoiva.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top