Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: MIGOGORO YA ARDHI YAMTOA JASHO MKUU WA WILAYA AKIMBIZANA KUTEKELEZA AGIZO LA PM
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
Mkuu wa wilaya ya Karagwe Deodatus Kinawiro ametekeleza agizo la Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania alilolitoa hivi ...




Mkuu wa wilaya ya Karagwe Deodatus Kinawiro ametekeleza agizo la Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania alilolitoa hivi karibuni la kumaliza mgogoro wa ardhi kati ya wananchi wa kijiji cha Kishoju na Dayosisi ya Karagwe mgogoro  ambao ulianza tangu mwaka 1980 ukihusisha hekta 422 zilizochukuliwa na Dayosisi.

Akiongea wananchi wa kijiji cha Kishoju leo Kinawiro amesema kuwa yeye ni kiongozi ambaye anatumikia wananchi wote kwa kufuata misingi ya sheria ,kanuni na taratibu za nchi ambapo amewaeleza wananchi kuwa wakati wa kugawa ardhi hiyo kwa Dayosisi ya Karagwe utaratibu wote ulifuatwa na hadi kuwapatia hati miliki hivyo hadi sasa inafahamika kuwa ardhi hiyo ni mali ya Dayosisi na wananchi wote ambao wako katika maeneo hayo wanatakiwa kutoka ili shughuli za Dayosisi ziweze kuendelea kwani ni kwa ajili ya maeneleo ya Wanakaragwe wote.


Kinawiro amesema kuwa ifikie wakati sasa wananchi waachane na migogoro isiyokuwa ya lazima na badala yake wajikite katika shughuli za maendeleo ambazo ziko mbele yao,kwani migogoro ambayo wanaiendekeza haitakuwa na msaada kwao katika maisha ya baadae.
Hata hivyo maamuzi ya mkuu wa wilaya hayakuwaridhisha wananchi wengi na viongozi wa serikali ya kijiji hicho huku wakieleza kuwa kwa sasa wakitolewa katika maeneo hayo ambayo wanafanyia shughuli zao za kilimo hawatakuwa na sehemu nyingine ya kwenda japo malalamiko hayo yametupiliwa mbali na mkuu wa wilaya akieleza kuwa hakuna anayetakiwa kuendele kufanya shughuli katika ardhi hiyo isipokuwa Dayosisi peke yake.

Hata hivyo Askofu wa Dayosisi Karagwe Bensoni Bagonza ameeleza utaratibu wote uliofuatwa hadi wanapata ardhi hiyo  ambapo walipewa tarehe 22 mwezi 12 mwaka 1980 na uongozi wa halmshauri wakati huo ndio ulisimamia zoezi la kuweka mipaka katika ardhi

Pia mkuu wa wilaya ya ameagiza mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Karagwe kuanzi hivi sasa kufanya mpango wa matumizi bora ya ardhi ili kuhakikisha hapaibuki migogoro mingine ya ardhi isiyokuwa



About Author

Advertisement

Post a Comment

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top