Wananchi kata ya Kayanga
Wilayani Karagwe wametaadhalishwa kuwa makini
katika maeneo wanakopita baada ya utapeli ambao umeonekana kuibuka na kuwaumiza baadhi
ya wafanyabiashara na watu wengine.
Hayo yamebabinishwa na
mwenyekiti wa KATOMA RUZINGA Amos Kahwa
katika mahojiano maalum ambapo ametaja suala la utapeli kuwa tatizo
kubwa kwenye kata hiyo.
Amos amesema kuwa katika
kipindi kifupi cha mwezi machi matukio kadhaa ya utapeli yamekuwa yakiripotiwa
hususan katika maduka ya Mpesa huku akitaja vijana ambao wengi wao ni wanafunzi
wa ngazi ya sekondari kuhusika kwa wingi katika utapeli huo.
Hata hivyo ametoa wito kwa
wananchi katika kata ya kayanga na wilaya ya karagwe kwa ujumla kuwa makini na
mali zao na watoe taarifa katika ofisi za kata na jeshi la polisi katika
kuhakikisha kuwa wahalifu hao wanapatikana.
Sambamba na hayo ametoa rai
kwa vijana wasiokuwa na shughuli maalum katika kata yake kurudi vijijini mara
moja kabla hawajakamatwa na kutiwa nguvuni na jeshi la polisi.
Katika hatua nyingine
amewataka wamiliki wa nyumba za kukodisha kuhakikisha kuwa wanatoa taarifa juu
ya kaya zao kwa kutoa taarifa muhimu za wapangaji wao kwa mwenyekiti wa mtaa
husika.
Post a Comment