Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: WANA IHEMBE TWO WAVUNJA SANDUKU HISA NI MKOMBOZI ZIPO TENA KIBAO ASIYEPENDA HISA.........
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
  Wananchi   wametakiwa   kujiunga   kwenye   vikundi   vya   vikoba   ili   waweze   kuinua   kipato   chao   kwa   kununua   hisa   ...
 
Wananchi  wametakiwa  kujiunga  kwenye  vikundi  vya  vikoba  ili  waweze  kuinua  kipato  chao  kwa  kununua  hisa  na  kusaidia  jamii  kwa  watu  wenye  uhitaji  kwenye  maeneo  yao.

Wito  huo  umetolewa  na  wanakikundi  cha  WAPENDANAO  cha  kijiji  cha  Ihembe two  wilayani  Karagwe  katika  sherehe  za  kuvunja  sanduku  na  kuanza  mwaka  mpya  wa  kununua  hisa  za  Kikundi  hicho.

Kikundi  cha  WAPENDANAO kilichoanzishwa  mwaka  2012  kikiwa  na  wanachama   8  sasa  kiendelea  kukua  na  kujiwekea  malengo  mbalimbali  kwa  kuanzisha  miradi  kadhaa  ya  kusaidiana  na  kusaidia  jamii  pia  ikiwemo kuwasaidi  hata  watoto  yatima.





Katika  risala  ya  kikundi  hicho  cha  WAPENDANAO  wanayo  miradi  kadhaa  ikiwemo  ufugaji  nyuki,mbuzi  na  kina  utaratibu  kwa  kulinda  na  kuendeleza  nidhamu  ndani  ya  kikundi  hicho.

Risala  hiyo  ilibainisha  pia  msaada  wanaoupata  kutoka  ulezi  wa  Kanisa  la  Kiinjili  la  Kilutheri  Tanzania  KKKT  dayosisi  ya  Karagwe.

Mkuu  wa  wilaya  ya  Karagwe  Deodatusi  Kinawiro  ndiye  alikuwa  mgeni  rasmi   ambapo  amewakilishwa  na  Katibu  tawala  wa  wilaya  Mustapha  Said  amesema  kikundi  hicho  kina  sifa  zote  za  kukopesheka  hivyo  kitaweza  kufikiriwa  na  serikali.

Hata  hivyo  wanakikundi  hicho  wameomba  ushirikiano  na  Idara  ya  maendeleo  iendelee  kuwalea  kama  ambavyo  inafanya  hivi  sasa  kwani  kuwepo  kwao  ni muhimu.


























About Author

Advertisement

Post a Comment

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top