Chama cha
ushirika cha Nguvumali
kimeshindwa kununua kahawa
msimu huu wa 2016/2017 kwa madai
ya wanachama 117
waliopewa mkopo kutoka
shirika la hifadhi
ya Jamii NSSF
Kushindwa kurejesha mkopo
huo kwa wakati
hivyo kukosa fedha
za kununulia kahawa.
Akizungumza na
chombo hiki kwa
njia ya simu
mwenyekiti wa Nguvumali
XAVERY France amesema
kuwa kutokana na
baadhi ya wanachama
kushindwa kurejesha mkopo
huo imekuwa ni
vigumu kukopa tena fedha
kwenye taasisi za
fedha kwa ajili
ya kununua kahawa
kwasababu bado wanadaiwa
na NSSF amesema
walipatiwa kiasi cha
shilingi million 950 na kuwakopesha
wanachama lakini imekuwa
vigumu kurejesha.
France amesema
kutokana na hali
hiyo wanachama wa Nguvumali
kupitia mkutano mkuu
walipitisha azimio la
kuwapeleka mahakamani wanachama
waliokopa na kushindwa
kurejesha fedha hizo
ambapo ameeleza kuwa
baadhi yao mahakama
imeishatoa hukumu na
julai 23 mwaka
huu dalali wa mahakama
yaani Court Breka
atawasilisha kusudio la kukamata
mali za wanachama
hao na kuzipiga
mnada.
Amesema kutokana
na hali hiyo
tayari shirika la
hifadhi ya Jamii
NSSF limetoa muda
wa kufikia hadi
tarehe 20 mwezi
wa nane kuhakikisha
mkopo huo uwe
umerejeshwa.
Post a Comment