Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: WANANCHI WA MAMLAKA YA MJI MDOGO WA KAYANGA WATAKIWA KUPIMA VIWANJA VYAO
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
Wananchi   katika mamlaka ya mji mdogo wa Kayanga wilayani Karagwe mkoani Kagera wametakiwa kuchangamkia fursa ya kupima viwanja vyao il...

Wananchi  katika mamlaka ya mji mdogo wa Kayanga wilayani Karagwe mkoani Kagera wametakiwa kuchangamkia fursa ya kupima viwanja vyao ili kuepuka migogoro ya ardhi isiyokuwa ya lazima inayojitokeza mara kwa mara.

Wito huo umetolewa leo na mkurugenzi wa Kampuni ya Mataro Land developers Tanzania Limeted  iliyoko jiji Mwanza inayojihusisha na upimaji wa ardhi  Joeli Mataro 


Mataro amesema kuwa kuna faida nyingi za kupima kiwanja mojawapo ikiwa ni kuepuka migogoro ya ardhi isiyokuwa ya lazima ambayo imekuwa ikijitokeza katika sehemu mbalimbali hapa Tanzania.

Mataro ametaja taratibu ambazo mwananchi anatakiwa kuzifuata endapo ataamua kupima kiwanja chake huku akieleza kuwa hadi sasa gharama za upimaji wa viwanja zimepungua na kufikia kiasi cha shilling laki mbili ambayo kila mwananchi na uwezo wa kuipata.


Kwa upande wake  kaimu mwenyekiti wa mamlaka ya mji mdogo wa Kayanga ambaye pia ni mwenyekiti wa Kijiji cha Katoma Ruzinga Amosi Kahwa amesema kuwa asilimilia 90 ya wananchi katika mamlaka ya mji mdogo wa Kayanga hawajapima viwanja vyao hivyo kuwataka kuitikia wito wa kuanza kufanya hivyo ili kukwepa usumbufu utakaojitokeza hapo baadae.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top