Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: WAZAZI NA WALEZI WAMETAKIWA KUWAANDAA WATOTO WAO WALIOHITIMU ELIMU YA MSINGI
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
Wazazi na   walezi   wa   wanafunzi   waliohitimu   elimu   yao   ya   msingi   wametakiwa kuwafundisha   elimu   ya   kujitegemea   kwa...

Wazazi na  walezi  wa  wanafunzi  waliohitimu  elimu  yao  ya  msingi  wametakiwa kuwafundisha  elimu  ya  kujitegemea  kwa  kipindi  ambacho  watakuwa  nyumbani  wakisubilia  matokeo  ya  mtihani  wao  walioufanya  mwezi  huu  amesema  kuwafundisha  kujitegemea  kutawasaidia  kwenye  maisha  yao ya  baadae.

Wito  huo  umetolewa  na Exvery  Buguzi  diwani  wa  Kata  ya  Nyakakika  ambaye  alikuwa  mgeni  rasmi  katika  maafali  ya  15  ya  shule  ya  Kiingereza  ya  Omukaliro  ambayo  ipo katika  kata  ya  Nyakabanga  wilayani  Karagwe  amesema  kuwa wanafunzi  waliohitimu  elimu  yao  ya  msingi  inabidi  kuwafundisha  kujitegemea  ili  waweze  kuwa wanajamii  wazuri  wa  baadae.

Amesema kuwa  hata  wanafunzi  waliohitimu  elimu  ya  msingi  mwaka  huu  waendelee  kujikumbusha  waliofundishwa  kama  maandalizi  ya  kuendelea  na  masomo  ya  sekondari  hapo  mwakani  hivyo  akawataka  wazazi  na  walezi  kujiandaa  na  hatua  hiyo  ambayo  ni  muhimu  kwa  watoto  wao kuendelea  na  ngazi  nyingine  hatimaye  wafikie  malengo  na  ndoto  zao.

Buguzi  amesema  wanafunzi  waliohitimu  wajihadhari  na  vitendo  visivyokubalika  katika  jamii  kama  uvutaji  bangi,ulevi,uzinzi   na  vitendo  vingine  ambavyo  haviendani  na  mila  na  utamaduni  wa  jamii  hivyo  wanatakiwa  kuepuka  visawishi  hivyo.

Aidha  amesema  kuwa ombi  la  wahitimu  waliolitoa  kupitia  risala  yao  ya  kutaka  shule  hiyo  iingizwe  kwenye  mpango  wa  umeme  vijijini  yaani   REA  amehaidi  kuendelea  kulifanyia  kazi  kwani  shule  hiyo  ni  taasisi  muhimu inayowasaidia  kuelimisha  watoto  wa  Tanzania

Akitoa  neno  la  shukrani  Mtume  Mstaafu  ambaye  pia  ni  mwenyekiti  wa  Karadea  Mathias Nzarombi amesema   wazazi  na  walezi  waendelee  kuwa  na  imani  na  shule  ya  OMUKALIRO  kwani  amazingira  ya  kujifunzia  na  kufundishia  ni  rafiki  kwa  watoto    na  kuonya  wapinzani  wao  kutowapiga  vita  visivyokuwa  na  maana  wala  ugomvi  wowote.

Hata  hivyo  waliohitimu  mwaka  huu  katika  shule  ya  Kiingereza  ya  Omukaliro  ni 31  ambapo  wasichana  ni   kumi  na  wawili  na  wavulana  ni  kumi na  19

About Author

Advertisement

Post a Comment

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top