Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: MADUKA 14 YATEKETEA KWA MOTO JIJINI ARUSHA
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
  Moto umeteketeza maduka maduka 14   katika eneo la Mianzini jijini Arusha. Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Arusha, Charles Mku...
 
Moto umeteketeza maduka maduka 14   katika eneo la Mianzini jijini Arusha.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Arusha, Charles Mkumbo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kutaja chanzo cha moto huo ulitokana na hitilafu ya umeme iliyoanzia kwenye majokofu yaliyokuwa yamehifadhiwa katika duka mojawapo lililoteketea kwa moto.

Alisema kwamba Moto huo ulianza majira ya saa 11:30 asubuhi ambapo ambapo ulisambaa na kushika mitungi ya gesi iliyolipuka na kusababisha kusambaa kwa kasi na kutekeketeza mali mbalimbali ambazo thamani yake bado haijajulikana.

Baadhi ya mashuhuda wanasema ya kwamba moto huo ulianzia kwenye duka kubwa Mianzini ambapo wamelaumu zimamoto kwamba endapo wangewahi kwenye eneo la tukio hilo wangeweza kuokoa baadhi ya mali zilizoteketea kwa moto.


About Author

Advertisement

Post a Comment

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top