Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: TISHIO LA NJAA WANANCHI WATAKIWA KUPANDA MAZAO YANAYOKOMAA KWA MUDA MFUPI
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
Wananchi wametakiwa kupanda mazao ya chakula yanayokomaa kwa muda mfupi ili kujikinga na njaa ambayo inaweza kusababishwa na mabad...



Wananchi wametakiwa kupanda mazao ya chakula yanayokomaa kwa muda mfupi ili kujikinga na njaa ambayo inaweza kusababishwa na mabadiliko ya hali ya hewa.


Rai hiyo imetolewa leo na mwenyekiti wa kijiji cha Amulama kata ya Kamagambo wilayani Karagwe Jackson Bitungwaramile  wakati akiongea na Karagwe    Forum


Jackson amesema kutokana na mabadiliko ya tabia ya nchi kila mwanajamii anatakiwa kupanda mazao yanayovumilia ukame na kusitawi kwa muda mfupi katika kujiwekea taadhali ya chakula hapo baadae.

 Amesema kwa yeyote atakayeshindwa kufanya hivyo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake maana wanaweza kusababisha Kaya  nyingi kukosa chakula.

Hata  hivyo  Mwenyekiti  wa  halmashauri  ya  wilaya  ya  Karagwe  wiki  hii  alitoa  kauli  kuwa  kila  Kaya  kuwa  na  hekali  moja  ya  viazi  vitamu  na  tayari  watendaji  wa  kata  wameishaagizwa  kusimamia  hilo  na  Kaya  itakayoshindwa  kufanya  hivyo  hatua  kali  za  kisheria  zitachukuliwa.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top