Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: MGODI WA DHAHABU WA GGM UMETOA MSAADA WA MADAWATI 4000 KWA WILAYA YA GEITA
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
Mgodi wa dhahabu wa Geita umechangia madawati 4,000 yenye thamani ya shilingi million 266 kwa Wilaya ya Geita. Madawati hay...





Mgodi wa dhahabu wa Geita umechangia madawati 4,000 yenye thamani ya shilingi million 266 kwa Wilaya ya Geita.

Madawati hayo yatakayotolewa kwa awamu mbili  za mwaka wa masomo yatapunguza adha kubwa inayowakabili wanafunzi wa halmashauri ya Wilaya hiyo na idadi kubwa ya wanafunzi walioandikishwa kwa mwaka wa masomo 2016 baada ya sera ya Elimu bule kutangazwa.

Pamoja na uchangiaji wa madawati ,Halmashauri hiyo inauhaba wa vyumba vya 56 vya  madarasa,ikilinganishwa na uwiano wa wanafunzi kwa kila mkondo .

Mradi huo wa madawati ni moja ya shuguli za kukuza uhusiano wa ujirani mwema kati ya jamii inayozunguka  mgodi wa GGM  ,ambapo tayari ujenzi wa karakana za uchomeleaji na mafunzo ya utengenezaji wa matofali ya kisasa unaendelea mjini Geita.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top