Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: MKOA WA KAGERA WASHINDWA KUTEKELEZA AGIZO LA RAIS JUU YA MADAWTI SHULENI
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
MKOA wa KAGERA umeshindwa kutekeleza agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania JOHN MAGUFULI kuhakikisha ifikapo Juni 30 mwaka huu as...
MKOA wa KAGERA umeshindwa kutekeleza agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania JOHN MAGUFULI kuhakikisha ifikapo Juni 30 mwaka huu asiwepo mwanafunzi anayekaa chini katika shule za msingi na sekondari kutokana na ukosefu wa madawati.

Kutokana na agizo hilo la Rais Magufuli alilolitoa wakati akiwaapisha wakuu wa mikoa mapema mwaka huu, mkoa wa KAGERA  ulipaswa kutengeneza madawati 73,874 ili kutimizia mahitaji ya madawati 200,439.


Madawati yaliyopaswa kutengenezwa yanajumuisha ya shule za msingi 64,601 na sekondari 9,273, lakini yaliyotengenezwa ni 35,956 yakiwamo ya shule za msingi 30,960 na ya sekondari 4,996. Upungufu uliopo sasa ni madawati 37,918.


Kufuatia jitihada zilizofanywa na serikali za kuhakikisha madawati yanayopungua yanataengenezwa, mkuu wa mkoa wa Kagera Meja
  Jenerali Mstaafu SALUMU  MUSTAPHA  KIJUU amewapongeza  wananchi wote mkoani hapa, taasisi za serikali na binafsi na makampuni yaliyoguswa na kuchangia madawati hayo.

Aidha ameendelea kuhamasisha kila mwananchi au taasisi itakayoguswa na suala hili la uchangiaji wa madawati kuendelea kuchangia, ili tumalize tatizo la watoto  kukaa chini, na kuwawezesha kupata elimu bora katika mazingira rafiki ya kujifunzia.


Ametaja  baadhi ya changamoto zilizochangia kutokamilika kwa utengenezaji wa madawati kwa wakati kuwa ni pamoja na kuwapo kwa tafsiri duni ya dhana ya elimu bila malipo na kufanya wananchi mwanzoni kuanza kusuasua kuchangia.


Changamoto nyingine ni kutumia muda mwingi kusubiri mbao kukauka na kutokuwa na umeme wa uhakika kwani madawati mengi yanatengenezwa kwa fremu za chuma katika wilaya ya Ngara, na kuwa halmashauri ambazo bado hazijakamilisha, zitakamilisha zoezi hilo kabla ya Julai 30 mwaka huu.


Hata hivyo katika utengenezaji huo, manispaa ya Bukoba imevuka lengo kwa kutengeneza madawati 244 ya ziada, na kufanya yaliyopo sasa kufikia 8,776 badala ya 8,532 yaliyohitajika.


About Author

Advertisement

Post a Comment

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top