Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: WATANZANIA WATAKIWA KUJIELIMISHA JUU YA MPANGO WA MAENDELEO ENDELEFU.
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
Watanzania wameaswa kujielimisha ili kushiriki kikamilifu katika kufanikisha mpango wa maendeleo Endelevu   ambao unalenga kuikwamua nch...

Watanzania wameaswa kujielimisha ili kushiriki kikamilifu katika kufanikisha mpango wa maendeleo Endelevu  ambao unalenga kuikwamua nchi katika umaskini na kukuza uchumi.

Hayo yamesemwa na Afisa Habari wa kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Usia Nkhoma Ledama  wakati akizungumza na MTANDAO HUUkwa lengo la kuhamasisha wananchi kutembelea banda la Umoja wa Mataifa (UN) katika maonesho ya 40 ya Biashara Jijini Dar es salaam  na kujifunza Malengo 17 ya Maendeleo Endelevu SDGs pia kujua shughuli mbalimbali zinazofanywa na Shirika hilo hapa nchini.


Aidha  Usia Nkoma ameeleza lengo la UN kuwepo katika Maoneosho hayo ya Biashara.



Katika kuelekea kilele cha Maonyesho ya 40 ya Biashara ya Kimataifa Sabasaba, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ametembelea banda la Umoja wa Mataifa (UN) lililopo katika ukumbi wa Karume kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere barabara ya Kilwa jijini Dar akiwa mgeni wa kwanza mashuhuri kutembelea banda hilo na kutoa baraka zake kwenye maonyesho hayo.



Amapo Nkoma amepongeza hatua ya kiongozi huyo na kuwahamasisha viongozi wengine kuiga mfano wake kwenda kuvuna maarifa kutoka umoja wa mataifa UN kwa ajili ya elimu kwa wananchi wake.

Hata hivyo ametoa wito kwa wananchi kujenga mahusiano mazuri na umoja huo sambamba na kuwa Karibu nalo ili waweze kujikwamua kiuchumi, kijamii, kisiasa na kiutamaduni kwani shirika hilo limekuwa likijikita katika katika kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili jamii.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top