Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: TIMU YA WATAALAM WA UJENZI KUTOKA NCHINI CHINA YAKAGUA ENEO LA UJENZI WA CHUO CHA VETA KAGERA ILI KUANZA UJENZI MARA MOJA
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
Na: Sylvester Raphael Serikali ya Watu wa China yatuma   timu ya Wataalam   wa Usanifu wa Majengo na   ujenzi   kukagua na kujiridhi...

Na: Sylvester Raphael


Serikali ya Watu wa China yatuma  timu ya Wataalam  wa Usanifu wa Majengo na  ujenzi  kukagua na kujiridhisha na eneo lililotengwa na Serikali ya Mkoa wa Kagera kwa ajili ya ujenzi wa Chuo cha Kisasa cha Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) kinachotarajiwa kujengwa  kwa ufadhili wa Serikali ya Watu china Mkoani Kagera katika Kijiji cha Burugo  Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba.




Timu hiyo ya Wataalamu kutoka katika Kampuni ya ujenzi ya “China Qiyuan Enginering Coorparation” ikiongozwa na Bw. Fang Ke Feng  walimueleza Mkuu wa Mkoa Kagera Ofisini kwake walipofika kumsalimia kuwa wamekuja kuona eneo la chuo cha VETA kitakapojengwa ili waweze kuchora michoro ya majengo inayoendana na eneo husika.



Baada ya kufika katika eneo la Burugo kitakapojengwa Chuo cha VETA Mkoa wa Kagera Wataalam hao kutoka nchini China  wakiongozwa na Msanifu Majengo Bw. Fang Ke Feng waliridhishwa na eneo hilo na kusema kuwa ni eneo zuri linalofaa kwa ujenzi na michoro wanayotarajia kuichora itaendana na eneo hilo.
“Tumeona eneo ni zuri sana, Serikali ya Mkoa imefanya kazi yake ya kufikisha miundombinu ya umeme na barabara katika eneo la ujenzi, pia tumeridhika na juhudi zinazoendelea kufanyika ili kuhakikisha maji yanapatikana katika eneo hili na jambo lakufurahisha Ziwa Victoria lipo karibu sana kwa upatikanaji wa maji katika ujenzi,” Alieleza Bw. Fang Ke Feng.


Vilevile kiongozi wa Timu hiyo ya wataalamu kutoka Nchini China Bw. Fang Ke Feng alisema kuwa baada ya kuona eneo husika sasa itachukua muda wa miezi miwili kabla ya ujenzi kuanza kutoka sasa ambapo watasanifu  michoro ya majengo na kuiwasilisha Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia ili iidhinishwe na ujenzi utaanza mara moja.


Kaimu Mkurugenzi wa Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Bw. Enock Kayani alisema kuwa ujenzi wa chuo hicho utagharimu jumla ya Shilingi bilioni 22.4 pia katika awamu ya kwanza  chuo kitadahili wanafunzi 400 na awamu ya pili wanafunzi 400 na kukamilisha jumla ya wanafunzi 800 mara baada ya chuo hicho kuwa kimekamilika.


Pia Bw. Enock alisema kuwa tayari Serikali imeanza kuwaandaa wakufunzi  wa ufundi katika chuo cha VETA Morogoro ili kujiandaa mapema kwaajili ya kuwafundisha wanafunzi watakaodahiliwa katika chuo cha VETA Kagera. 


Pia alisistiza kuwa Walimu hao watapelekwa nchini china kujifunza zaidi kwani mara baada ya Chuo kukamilika kitakuwa na Mashine za kisasa zinazohitaji ujuzi zaidi.


Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum M. Kijuu akiongelea ujio wa wataalam hao kutoka nchini China alisema amefurahishwa sana na ujio wao kwani uongozi wa mkoa na wananchi kwa ujumla wamekuwa wakisubiri kwa hamu kubwa ujenzi wa chuo hicho kuanza na Serikali ya mkoa tayari imefanya majukumu yake ya kuhakikisha miundombinu ya umeme na barabara imefika katika eneo husika.

Mwenyekiti wa Kiji ji Burugo  Bw. Samson K. Simon akiongea na Timu ya Wataalamu kutoaka Nchini China Alisema kuwa imekuwa furaha kubwa kwake na wanakijiji wa Burugo kwani wamekuwa wakisubiria kwa hamu sana ujenzi wa chuo hicho kuanza na ni matarajio yao kuwa watapata ajira mbalimbali za kuinua vipato vyao pia ujenzi wa chuo hicho utainua sana uchumi wa kijiji chao.


Katika hatua nyingine Timu ya Wataalamu kutoka nchini China ilipata wasaa wa kutembela Shule ya Sekaondari Ihungo iliyopo Manispaa ya Bukoba inayojengwa upya na Serikali ya Tanzania mara baada ya kuharibiwa vibaya na Tetemeko la Ardhi lililotokea Septemba 10, 2016. 


Lengo la Timu hiyo kufanya ziara katika Shule ya Sekondari Ihungo ni kujionea ubora wa majengo yanayojengwa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA).

About Author

Advertisement

Post a Comment

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top