Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: MFANYABIASHARA BUKOBA KAGERA ANASWA NA TANI MBILI ZA SUKARI PAMOJA NA POMBE HARAMU
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
Jeshi la polisi mkoani KAGERA linamshikilia mfanyabiashara mmoja wa manispaa ya BUKOBA mkazi wa kata Rwamishenye kwa kuhifadhi...





Jeshi la polisi mkoani KAGERA linamshikilia mfanyabiashara mmoja wa manispaa ya BUKOBA mkazi wa kata Rwamishenye kwa kuhifadhi sukari tani mbili huku  wananchi wakiwa wanaendelea kukosa sukari katika maeneo mbalimbali


Akizungumza na waandishi wa habari  kamanda wa jeshi la polisi mkoani KAGERA AGUSTIN OLLOMI amemtaja anayeshikiliwa ni BENEDICTO BUCHARD ambaye alikuwa ana mifuko 80.

Amebainisha kuwa mtu anayefanya hivyo anawanyanyasa wananchi wenzake ikiwa wanakosa sukari madukani huku yeye akificha sukari ili awauze kwa gharama ya juu.


Katika hatua nyingine mfanyabiashara huyo amekamatwa na pombe haramu aina ya viroba ambavyo vimezuiliwa kuingizwa nchini.

Kwa mujibu wa kamanda OLLOMI amesema kuwa pombe hizo zinatoka nje ya nchi na mfanyabiashara huyo ameingiza pombe hizo kinyume na sheria.


About Author

Advertisement

Post a Comment

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top