Takwimu za hivi karibuni
hapa nchini zinaonyesha kwamba kwa mwaka, Tanzania inapoteza kina mama 7,900
kutokana na sababu zitokanazo na ujauzito ambapo Idadi hiyo ni sawa na vifo 22
kwa siku.
Magonjwa yanayoongoza
kusababisha vifo vya wazazi nchini na mataifa mengine ni kifafa cha mimba,
uzazi pingamizi, kupoteza damu nyingi wakati na baada ya kujifungua na
maambukizi baada ya kujifungua.
Ofisa Mawasiliano wa
Muungano wa Utepe Mweupe kwa Uzazi Salama, Lydia Kamwaga amesema taarifa nyingi
zimeonyesha bado vituo vingi vya afya havitoi huduma za uzazi za dharura
kutokana na ukosefu wa vifaa kama vile vya upasuaji.
Waziri wa afya, maendeleo ya jamii, jinsia,
wazee na watoto Ummy Mwalimu, ameipongeza zahanati ya Uturo wilayani Mbarali
Mkoani Mbeya kwa kuwa imekuwa mfano wa kuigwa Nchini Tanzania kwa kuzuia vifo
vitokanavyo na mama wajawazito na watoto wachanga.
Aidha, amesema anautambua mchango mkubwa
kwa watoa huduma ngazi ya jamii na kwamba Moja ya kipaumbele chake katika
wizara hii ni kupunguza vifo vinavyoweza kuzuilika.
Kwa upande wao baadhi ya wakinamama ndani
ya wilaya ya kyela wameeleza sababu zinazotokana na vifo kwa wanawake na watoto
pindi walipohojiwa na kituo hiki juu ya sababu zinazosababisha vifo hivyo
kushamiri hapa nchini.
Hata hivyo ili kupunguza vifo hivyo
inashauriwa kuweka mikakati ya kuzuia akina mama kujifungulia nyumbani na kila
mwanaume na mwenza wake kuhakikisha wanahudhuria kliniki kuanzia ujauzito hadi
mtoto anapofikisha umri wa miaka mitano.
About Author
The part time Blogger love to blog on various categories like Web Development, SEO Guide, Tips and Tricks, Android Stuff, etc including Linux Hacking Tricks and tips. A Blogger Template Designer; designed many popular themes.
Advertisement

Related Posts
- KAGERA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA VYAFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KUENDELEA KUJIIMARISHA KUWALINDA RAIA NA MALI ZAO25 Apr 20180
Na: Sylvester Raphael Vyombo ya Ulinzi na Usalama Mkoani Kagera vyafanya mazoezi ya ...Read more »
- MBIO ZA MWENGE WA UHURU KATIKA WILAYA ZA KARAGWE NA NGARA PIA HITIMISHO WILAYANI BIHARAMULO MKOANI KAGERA16 Apr 20180
Na: Sylvester Raphael Mwenge wa Uhuru waendelea kuchanja mbuga Mkoani Kagera kwa ku...Read more »
- MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MKOANI KAGERA NA KUANZA UZINDUZI WA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI YA ZAIDI YABILIONI 1216 Apr 20180
Na: Sylvester Rapahel Mwenge wa Uhuru umepokelewa leo April 8, 2018 Mkoani Kagera na...Read more »
- TIMU YA WATAALAM WA UJENZI KUTOKA NCHINI CHINA YAKAGUA ENEO LA UJENZI WA CHUO CHA VETA KAGERA ILI KUANZA UJENZI MARA MOJA16 Apr 20180
Na: Sylvester Raphael Serikali ya Watu wa China yatuma timu ya Wataalam wa Usanif...Read more »
- MKOA WA KAGERA WAVUKA LENGO KATIKA UNDIKISHAJI WA WANAFUNZI AWALI NA DARASA LA KWANZA MWAKA 201816 Apr 20180
Na: Sylvester Raphael Mkoa wa Kagera wavuka lengo la uandikishaji wa Wananfunzi katika madarasa...Read more »
- MKUU WA MKOA KAGERA AAGIZA MKANDARASI KUKAMATWA NA KUFIKISHWA OFISINI KWAKE AKIWA NA PINGU MIKONONI BAADA YA KUITIA SERIKALI HASARA08 Mar 20180
Na Sylvester Raphael Mkuu wa Mkoa wa Kagera aagiza Mkandarasi wa Kampun...Read more »
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.