Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: WATUMISHI HEWA KARAGWE KAA LA MOTO WATUMISHI 62 WABAINIKA SOMA ZAIDI HAPA
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
WATUMISHI    HEWA. Hadi   tarehe   30   April ,2016 wilaya   ya   Karagwe   ilikuwa   na   watumishi   hewa   62   kwa   mchanganuo   ...

WATUMISHI   HEWA.
Hadi  tarehe  30  April ,2016 wilaya  ya  Karagwe  ilikuwa  na  watumishi  hewa  62  kwa  mchanganuo  ufuatao.

A:WIZARA  YA  AFYA

HOSPITALI  TEULE  YA  NYAKAHANGA
.Watumishi  hewa 36 wanaolipwa   na  serikali  kuu  kupitia  wizara  ya Afya wamebainika  ni  Hewa.

Kwa  kipindi  cha  mwaka wa  fedha  2010/2011 hadi 2015/2016 fedha  zilizolipwa  ni  TSHS:609,785,800  baada  ya  kuondoa  makato  ya  kisheria.

.Uongozi  wa  hospital  umeagizwa  kurejesha  fedha  hizo 

.Aidha barua  zimepelekwa  wizara  ya  Afya ,Ofis  ya  Rais  Menejiment   ya  Utumishi wa  Umma  na Benki  ya  NMB ili  wachukue  hatua  stahiki.

B.HALMASHAURI YA  WILAYA
Watumishi 26  wamebainika  kuwa  ni  hewa  kwa  mchanganuo  ufuatao.

-Watumishi 22 wamebainika  kuwa  watoro  na  wameondolewa  kwenye “PAYROLL”
Watumishi 02(wawili) wamebainika kuwa  walistaafu  na  wameondolewa  kwenye  PAYROLL,fedha  zimerudishwa

-Mtumishi 01  ( mmoja) amebainika  alifariki  dunia  tarehe 10 Februari ,2016 na  alikuwa  kwenye Payroll ya  mwezi  machi ,2016 Fedha  zilizochukuliwa  zimerudishwa
Mtumishi 01(Mmoja) amebainika  kuwa  na  cheki  namba  mbili.Fedha  zimerudishwa  kiasi  cha  Tshs 18,555,000

Kwa  ujumla fedha  zilizokuwa zinalipwa  kwa  watumishi  hewa TSHS 259,182 O50,27 kati  ya  hizo  zirizorejeshwa  ni TSHS 30,985,441.46

C TAASISI  ZINGINE  ZA  UMMA/SERIKALI
Mkuu  wa  wilaya ameunda kamati  ya  watu  wanne  kuhakiki taarifa  za  watumishi  hewa ndani  ya halmashauri  ya  wilaya ,serikali  kuu  na  taasisi  zote  za serikali /umma  zilizoko wilayani


About Author

Advertisement

Post a Comment

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top