Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: WAOKOLEWA BAADA KIVUKO KUPINDUKA NA MWINGINE MMOJA BADO HAJULIKANI ALIOPO.
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
Watu wapatao 30 wameokolewa mpaka sasa baada ya kivuko cha mto Kilombero kushindwa kuhimili upepo mkali ulioambatana na mvua ya radi ...

Watu wapatao 30 wameokolewa mpaka sasa baada ya kivuko cha mto Kilombero kushindwa kuhimili upepo mkali ulioambatana na mvua ya radi  na  kukifanya kigonge nguzo za pembeni ya mto na kukosa mwelekeo hivyo kupinduka ndani ya maji jana usiku.

Kwa mujibu wa taarifa rasmi ya serikali iliyotolewa leo Bungeni na Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera,Bunge,Kazi,Vijana ,Ajira na Walemavu) Jenista Mhagama, kivuko hicho kilikuwa  na  watu 31, magari na mizigo mbalimbali  ambapo  mpaka sasa  mtu  mmoja bado hajapatikana.

Tukio la kivuko hicho cha mto Kilombero kushindwa kumudu upepo sio mara ya kwanza kujitokeza katika eneo hilo la mpakani mwa wilaya za Kilombero na Ulanga, ambapo juzi hali kama hiyo ilijitokeza.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top