Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: WANANCHI WANAOTUMIA ZIWA VICTORIA WAMETAKIWA KUCHUKUA TAHADHARI KUEPUSHA AJALU
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
Wananchi  wanaotumia ziwa Victoria katika shughuli  mbalimbali ikiwemo uvuvi  wametakiwa kuchukua tahadhari  katika kipindi hiki ambapo ziwa...
Wananchi  wanaotumia ziwa Victoria katika shughuli  mbalimbali ikiwemo uvuvi  wametakiwa kuchukua tahadhari  katika kipindi hiki ambapo ziwa hilo limechafuka kwa kuwa na upepo mkali.


Kamanda wa polisi mkoani KAGERA AUGUSTINE  OLLOMI amesema hayo baada ya kuwepo kwa taarifa za matukio ya watu kufa maji katika ziwa hilo ambayo yanasababishwa na upepo.

Amesema kuwa,kumetokea matukio mawili tangu kuanza kwa mwezi june,ambapo katika tukio la kwanza  watu watatu walifariki huku tukio la pili likimhusisha mtu mmoja aliyekutwa mwili wake ukielea juu ya maji siku mbili baada ya kuaga nyumbani kuwa anakwenda kuvua samaki.


Hata hivyo amewataka wavuvi kutumia vifaa vya kujiokolea kama lifejacket pindi kunapotokea ajali ya mitumbwi yao kupigwa dhoruba au kuzama.


About Author

Advertisement

Post a Comment

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top