Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: WATU WAWILI WAPOTEZA MAISHA KATIKA MATUKIO MAWILI TOFAUTI MKOANI KAGERA
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
Watu wawili wamefariki dunia katika matukio mawili tofauti baada ya kujinyonga katika kata ya Nyanga na Buhembe manispaa ya Bukoba. Kamanda...
Watu wawili wamefariki dunia katika matukio mawili tofauti baada ya kujinyonga katika kata ya Nyanga na Buhembe manispaa ya Bukoba.

Kamanda wa polisi mkoani Kagera  AUGUSTINE OLLOMI amesema kuwa katika tukio la kwanza mtu mmoja aitwaye RAPHAEL IGNAS mwenye umri wa miaka 72 amekutwa kwenye shamba la jirani yake  akiwa amejingonya na kamba ya mgomba kwenye mti wa muembe.


Kamanda OLLOMI amesema kuwa,tukio la pili ni lile lililomhusisha RESPICIUS ELIMANI  mwenye umri wa miaka 45 ambaye amekutwa amejingonga nyumbani kwake  kwa kutumia kamba ya manira kwenye mti wa Mparachichi.


Aidha ameongeza kuwa mpaka sasa hakuna mtu anayeshikiliwa na jeshi hilo na chanzo cha vifo hivyo hakijajulikana hivyo polisi inaendelea na uchunguzi.


About Author

Advertisement

Post a Comment

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top