Halmashauri ya
wilaya ya Karagwe
Mkoani Kagera imefanikiwa
kupata gari la
zimamoto na linatarajiwa
kufika wilayani humu
ndani ya wiki
moja hii inaifanya
wilaya ya karagwe
kuwa miongoni mwa
halmashauri chache hapa
nchini kuwa na
gari la zimamoto.
Akizungumza kwa
nia ya simu
kutoka mjini Dodoma
anakohudhuria vikao vya
Bunge vinavyoendelea Mbunge
wa Jimbo la Karagwe
Innocent Bashungwa amesema
gari hilo tayari
limepatikana hivyo wananchi
wa wilaya ya
Karagwe waondoe shaka juu ya kutokuwepo
gari la Zimamoto.
Bashungwa amesema
anaishukuru serikali kuwa
sikivu kwa kukubali
ushauri na maombi
ya wilaya yaliyowasilishwa na
kuongeza kuwa anampongeza
pia mkuu wa
wilaya ya Karagwe
kwa Deodatus Kinawiro
kwa ushirikiano wake
alioutoa katika kufanikisha
kupatikana kwa gari
hilo.
Amesema halmashauri
nyingi hazina magari
ya zimamoto maana
ni ghali mno
kuzipata na kwa
wilaya ya Karagwe
wametumia ushawishi mkubwa
wa kuelezea kukua
kwa kasi mji
wa Kayanga na
uwepo wa viwanda
vya kukoboa kahawa
pia kutokana na
majanga ya moto
na hiyo imesaidia kujenga
usawishi wa kuhakikisha
kupata gari hilo.
Aidha Bashungwa
amesema changamoto nyingine
zinazoikabili wilaya ya
Karagwe ataendelea kuziwasilisha
serikalini pia kuishauri kuiangalia
Karagwe kwa jicho
la pekee.
Hata hivyo
amewataka wananchi wote
katika jimbo la
Karagwe kuendelea kufuatilia
na kutumia ushauri
unaotolewa na watalaamu
ili kuweza kuepuka
majanga yasiyokuwa ya
lazima.

Post a Comment