Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: WAFANYABIASHARA WATAKAONDA KINYUME NA BEI ELEKEZI YA SUKARI ILIYOTOLEWA NA SERIKALI
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
Mkuu wa mkoa wa Kagera Meja   Jeneral Mstaaf SALUMU KIJUU amesema kuwa atawachukulia hatua wafanyabiashara wote ambao wataenda kinyume n...

Mkuu wa mkoa wa Kagera Meja  Jeneral Mstaaf SALUMU KIJUU amesema kuwa atawachukulia hatua wafanyabiashara wote ambao wataenda kinyume na bei ya sukari iliyotolewa na serikali.


Akizungumza na vyombo vya habari KIJUU amesema atasita kuwachukulia hatua wale woteambao watajipangia bei ya sukari na kwenda na bei elekezi kutokana na kiwanda cha sukari cha kagera sukari kuacha kuzalisha sukari katika kipindi hiki cha mvua.



Amefafanua kuwa kutokana na kumuzuia wakala wa kusambazasukari kuacha kusambaza sukari katika mikoa ya jirani wananchi wanapaswa kutoa taarifa kupitia kamati ya ulinzi na usalama kama kutakuwepo na utoroshwaji wa sukari nyakati za usiku kwenda katika mikoa hiyo.




Aidha ametaja vigezo vilivyotumika kutambua maduka matatu matatu kila kata ya wafanyabiashara ambao watauza sukari kwa bei elekezi.



Hata hivyo  Meja  Jeneral Mstaafu KIJUU amesema kuwa sukari itarejea katika khali ya kawadaida mwezi wa sita ambapo sukari itaendelea kusambazwa katika mikoa jirani .

About Author

Advertisement

Post a Comment

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top