Zaidi ya milioni 545 zimetumika
kuwalipa watumishi hewa 99 mkoani KAGERA ikiwampaka sasafedha
zilizorudishwa na watumishi hao ni milioni60.
Akizungumza na vyombo vya habari
mkuu wa mkoa waKAGERA Meja Jeneral Mstaafu SALUMU KIJUU amesema kuwa watumishi
hao wamehakikiwa kipindi cha mach mpaka sasa ambapo waliobainika mpakasasa ni
hao 99.
Akitaja watumishi katika wilaya zote
zamkoa wa KAGERA amesema biharamulo ni watumishi hewa 9 manispaa ya bukoba
watumishi 7 ngara watumishi 3 bukoba halmashauri watumishi hewa 22
karagwe watumishi 26 huku muleba ikiwa na watumishi hewa 17.
Kutokana na huakiki huo mkoa
umeundabaraza ambalo litasaidia kuhakiki watumishi wotekwa ngazi za vijiji kata
na wilaya huku akibainisha kuwa badhi ya watumishi wanapokea mishahara mikubwa
kuliko kiwango chao.
Hata hivyo Meja Jeneral Mstaafu KIJUU amebainisha kuwa
baadhi ya watumishi katika idara za afya ni hewa lakini wameshindwa kuwaingilia
kutokana na baadhi ya vituo kusimamiwa na tasisi kama makanisa ambazo
aziishirikishi halmashauri husika.
Post a Comment