Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: WATUMISHI WATAKIWA KUJITUMA ZAIDI NA WAKITANGULIZA UADILIFU NA UWAJIBIKAJI
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
Watumishi   wametakiwa   kufanya   kazi   kwa uadilifu,uwajibikaji   na    kujituma   zaidi    ili   kuwatumikia   wananchi    na   wala...

Watumishi  wametakiwa  kufanya  kazi  kwa uadilifu,uwajibikaji  na   kujituma  zaidi   ili  kuwatumikia  wananchi   na  wala  watumishi  wasijione  wao  ni  maboss wamepewa  dhamana  hiyo  kuwatumikia  wananchi  kwa  ajili  ya  kutatua  kero  zao.


Kauli  hiyo  imetolewa  na Mkuu  wa Mkoa wa Kagera  Meja  Jenerali  Mstaafu  Salum  Mustapha  Kijuu  wakati  akiongea  na  watumishi  wa  kada  mbalimbali  wa  halmashauri  ya  Karagwe   hiyo  ikiwa  ni  ziara   ya  kujitambulisha  tangu  kuteuliwa  na  Rais  wa  Jamhuri  ya  Muungano  wa  Tanzania  Dk Jih Pombe  Magufuli.

Amesema  kuwa  zama  za  kutegea  kazi,kufanya  kwa  uzembe  na  kulindana  imepitwa  na  wakati  sasa  ni  awamu  ya   kazi  tu hivyo watumishi  watambue  hilo  na  wakizingatia  uwajibikaji  na  uadilifu  zaidi  na  atakayeshindwa  kuzingatia  hayo  hawatasita  kumuondoa  kwenye  nafasi  hiyo  mara  moja.


Mkuu  wa  Mkoa  Kijuu  amesetoa maagizo  ambayo  amesema  kuwa  yatakuwa  ni  kipimo  cha  utekelezaji  wa kazi kwa  kila  halmashauri  hapa  mkoani  Kagera  kwa  kipindi  cha  kuanzia  mwezi  huu  huku  akisisitiza  suala  la  ukusanyaji  mapato  kupewa  kipaombele  kikubwa  zaidi  huku  akionya   wanaokusanya   mapato  bila  kufikisha  pesa  benki.


Ametoa  muda  wa  siku  14  za  kuhakikisha  uongozi  wa  halmashauri kufanya  uthamini  wa  majengo  kwa ajili  ya  kupanga  kiwango  cha  ulipaji  kodi  ya  majengo  kwani  ni  chanzo  muhimu  cha  kuingizia  halmashauri  na  serikali  mapato pia  ameagiza  makusanyo  yote  ya  kodi  ya  halmashauri  utumie  mfumo  wa  kielectroniki  yaani  EFDs  kuanzia  mwezi  juni

Aidha    agizo  jingine  ni  utekelezaji  wa  maagizo  ya  serikali  kwa  wakati  na  halmashauri  ambayo  haitimiza  mikutano  ya  kisheria  itawajibishwa  na  kutoa  taarifa  zisizokuwa  sahihi  hazitavumiliwa .

Meja  Jenerali  Kijuu  ameagiza  pia  taarifa  ya  mkaguzi  na  mdhibiti  wa  hesabu  za  serikali  CAG  zitolewe  siku  21 zikiwa  na  viambatanisho  vyote  vinavyohitajika  ili  kuweza  kuepuka  kupata  hati  zenye  mashaka  au  chafu.

Katika  usimamizi  wa  shughuli  za  serikali  amemtaka  mkurugenzi  na  idara  ya  ujenzi  kuweka  wazi   maelezo  ya  mradi  unaanza  lini  unatarajia  kuisha  lina  pia gharama  za  mradi  huo  zianishwe  na  mkandarasi  ni  nani anayetekeleza  mradi  huo.


Hata  hivyo  ameutaka  uongozi  wa  halmashauri  ya  wilaya  ya  Karagwe  kukuna  vichwa  kwa  ajili  ya  kutenga  maeneo  ya  kuwawezesha  vijana  kufanya  kazi  kuliko  kuendelea  kuzurula  na kusema  hilo  atalifuatilia  kwa  karibu.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top