Home
»
News
» UJENZI WA CHUO CHA KISASA CHA UFUNDI STADI VETA KAGERA MBIONI KUANZA MARA MOJA BURUGO HALMASHAURI YA WILAYA YA BUKOBA
Na: Sylvester Raphael
Ujenzi
wa Chuo cha kisasa cha Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) Kagera wakaribia kuanza
katika eneo la Burugo Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba nje kidogo ya Manispaa ya
Bukoba ili kutoa Elimu au Mafunzo ya Ufundi Stadi kwa vijana wengi wanaohitimu
elimu ya Msingi na Sekondari kutoka ndani na nje ya mkoa.
Chuo cha Mafunzo ya Ufundi
Stadi (VETA) Kagera kinatarajiwa kujengwa kwa ufadhili wa Serikali ya China,
aidha, Serikali hiyo imetuma wataalam wa
sekta mbalimbali za ujenzi na tayari wamewasili mkoani Kagera kuanzia Septemba 7, 2016 ili kufanya upembuzi
yakinifu wa gharama za ujenzi wa chuo katika eneo kitakapojengwa.
Wataalamu hao wanane kutoka
nchini China waliwasili mapema asubuhi katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa kumsalimia
na kujitambulisha ambapo kati yao kuna Mhandisi wa masuala ya Maji, Ujenzi, na
Umeme ambao kwa mujibu wa kiongozi wao watafanya upembuzi yakinifu wa gharama
za ujenzi, katika eneo husika, mfano kuona eneo kama linafaa, upatikanaji wa
vifaa, gharama za vifaa na masuala yote yanayohusu ujenzi.
Mara baada yakuwapokea
ofisini kwake Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum M. Kijuu aliwaeleza
kuwa Serikali ya Mkoa ipo tayari kutoa ushirikiano kwao ili ujenzi wa chuo
hicho uanze mara moja . Pia liwakaribisha mkoani Kagera pamoja na kuja kufanya
upembuzi yakinifu lakini watembelee mkoa na kuona Kagera ilivyobarikiwa katika fursa
mbalimali za utalii na kiuchumi.
Chuo cha Kisasa cha Mafunzo
ya ufundi stadi (VETA) Kagera kinatarajiwa kujengwa na kuwa chuo cha mfano wa
vyuo vya ufundi nchini ambapo kitadahili wanafunzi wengi na kitakuwa na fani
mbalimbali za ufundi stadi ambazo zitakuwa zinaendana na hali halisi ya sasa ya
Sayansi na Technolojia .
Mkoa wa Kagera tangu
mwaka1987 hadi sasa hauna chuo cha (Vocational Educational and Training
Authority, VETA) cha ufundi isipokuwa kuna
Kituo cha mafunzo ya ufundi (Vocational Training Center) VTC Rwamishenye
ambacho ni kimojawapo kati ya vituo 27 vinavyomilikiwa na VETA chini ya Wizara
ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi nchini.
Kutokana na VTC kagera
kutokuwa na uwezo wa kudahili wanafunzi wengi aidha, kuwa kituo cha mafunzo
kisichokuwa na wanafunzi wa kulala (bweni) na kupelekea wanafunzi ambao ni wa nje
ya Manispaa ya Bukoba kukosa elimu ya ufundi na kuishia mitaani baada ya
kumaliza elimu ya msingi na sekondari ndiyo sababu Serikali ya Tanzania iliamua
kujenga chuo cha kisasa Kagera ili kupunguza tatizo hilo.
Ni baada ya Serikali ya
Awamu ya Nne chini ya aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete kuamua kujenga Chuo cha Kisasa
cha Ufundi, Rais Kikwete aliiomba nchi
rafiki ya China kujenga chuo hicho na kupendekeza kijengwa mkoani Kagera.
Aidha Rais Kikwete alitangza uamuzi wa Serikali ya
China kukubali kujenga chuo hicho cha Ufundi Stadi Mkoani Kagera Wakati
akiongea na wazee wa Mkoa wa Dodoma katika Ukumbi wa Kilimani tarehe 04/11/2014
na kuipongeza Serikali ya China kwa kukubali ombi lake kwa dhati.
Wananchi wa Mkoa wa Kagera hatuna budi kuupokea mradi wa
ujenzi wa chuo hicho kikubwa cha kisasa na kitakachotoa elimu ya ufundi wa
kisasa unaoendana na sayansi na teknolojia , pia na kutoa ajira kwa wananchi wa
mkoa wetu wakati wa ujenzi na mara baada ya kumalizika kujengwa kwa chuo hicho.
About Author
The part time Blogger love to blog on various categories like Web Development, SEO Guide, Tips and Tricks, Android Stuff, etc including Linux Hacking Tricks and tips. A Blogger Template Designer; designed many popular themes.
Advertisement

Related Posts
- KAGERA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA VYAFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KUENDELEA KUJIIMARISHA KUWALINDA RAIA NA MALI ZAO25 Apr 20180
Na: Sylvester Raphael Vyombo ya Ulinzi na Usalama Mkoani Kagera vyafanya mazoezi ya ...Read more »
- MBIO ZA MWENGE WA UHURU KATIKA WILAYA ZA KARAGWE NA NGARA PIA HITIMISHO WILAYANI BIHARAMULO MKOANI KAGERA16 Apr 20180
Na: Sylvester Raphael Mwenge wa Uhuru waendelea kuchanja mbuga Mkoani Kagera kwa ku...Read more »
- MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MKOANI KAGERA NA KUANZA UZINDUZI WA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI YA ZAIDI YABILIONI 1216 Apr 20180
Na: Sylvester Rapahel Mwenge wa Uhuru umepokelewa leo April 8, 2018 Mkoani Kagera na...Read more »
- TIMU YA WATAALAM WA UJENZI KUTOKA NCHINI CHINA YAKAGUA ENEO LA UJENZI WA CHUO CHA VETA KAGERA ILI KUANZA UJENZI MARA MOJA16 Apr 20180
Na: Sylvester Raphael Serikali ya Watu wa China yatuma timu ya Wataalam wa Usanif...Read more »
- MKOA WA KAGERA WAVUKA LENGO KATIKA UNDIKISHAJI WA WANAFUNZI AWALI NA DARASA LA KWANZA MWAKA 201816 Apr 20180
Na: Sylvester Raphael Mkoa wa Kagera wavuka lengo la uandikishaji wa Wananfunzi katika madarasa...Read more »
- MKUU WA MKOA KAGERA AAGIZA MKANDARASI KUKAMATWA NA KUFIKISHWA OFISINI KWAKE AKIWA NA PINGU MIKONONI BAADA YA KUITIA SERIKALI HASARA08 Mar 20180
Na Sylvester Raphael Mkuu wa Mkoa wa Kagera aagiza Mkandarasi wa Kampun...Read more »
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.