Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: MARUFUKU KUUZA AU KUNUNA KAHAWA YA MAGENDO KWA WILAYA YA KARAGWE
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
Maafisa watendaji wa kata na vijiji na wenyeviti wa vijiji na vitongoji katika kata zilizopo katika ukanda wa Bushangaro wilayani Karagw...

Maafisa watendaji wa kata na vijiji na wenyeviti wa vijiji na vitongoji katika kata zilizopo katika ukanda wa Bushangaro wilayani Karagwe mkoani Kagera wametakiwa kufuatilia na kupiga marufuku wanunuzi wa kahawa za magendo ambao tayari wameanza kuzunguka vijijini kwa wakulima kwa ajili ya kuwalaghai kuwauzia kahawa za magendo.

Wito huo umetolewa na mkuu wa kituo cha polisi Omukarilo wilayani Karagwe Antony Bupamba wakati akiongea na baadhi ya viongozi wa kata za Kibondo,Nyakabanga,na Nyakakika wilayani humu.

Bupamba amesema kuwa  tayari wanunuzi wa kahawa za magendo wameshaanza kupita kwa wakulima kwa ajili ya kununua kahawa  mbichi jambo ambalo ni kinyume na sheria ambapo amesema kuwa ni jukumu la viongozi wa vijiji kuhakikisha wanapambana na watu wanaofanya hivyo kwa kuwafikisha katika vyombo vya sheria.

Amesema kuwa watakaemkamata wamfikishe katika kituo cha polisi na hatua dhidi yake sitachukuliwa ikiwa ni pamoja na kulala ndani kwa muda wa masaa 24 ili iwe fundisho kwa watu wengine wanaofanya hivyo.

Nao wananchi waliongea na mtandao  huu wamekili kuwepo   kwa vitendo vya uuzaji wa kahawa za magendo huku wakijihusisha na vitendo vya uvunaji wa kahawa mbichi na kuanika chini jambo ambalo wamelitaja kuwa ni kutofuata ushauari wa wataalamu ambao wanaotoa kila siku.


Hata hivyo wamewataka wananchi kuacha kuitupia lawama serikali kwani kuzidi kushuka kwa bei ya kahawa kila mwaka ni kutokana na uvunaji mbovu wa kahawa ambao unasababisha kahawa kutokuwa na ubora.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top