Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: OKOA KARAGWE ISIWE JANGWA WADAU WAJIPANGA WAANZIA BUSHANGARO KUPANDA MITI
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
Wadau wa mazingira kwa kushirikiana na viongozi wa halmashauri ya wilaya ya Karagwe mkoani Kagera wameweka mikakati ya utunzaji w...




Wadau wa mazingira kwa kushirikiana na viongozi wa halmashauri ya wilaya ya Karagwe mkoani Kagera wameweka mikakati ya utunzaji wa mazingira  kwa kupanda miti katika maeneo yenye vipara ili kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi.

Wakiongea na viongozi ngazi ya vijiji na kata za Nyakakika,Nyakabanga,Kibondo, na Nyabiyonza  wamesema kuwa mabadiliko makubwa ya tabia ya nchi yanasababishwa na vitendo na shughuli za binadamu.
Mratibu wa mradi wa utunzaji wa mazingira wa Kanisa La Kiinjili la Kiruthel Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Karagwe Horace Kamkoto  ametaja baadhi ya shughuli za binadamu zinazochangia uharibifu wa mazingira na mabadiliko ya tabia ya nchi.

Afisa kilimo wilaya ya Karagwe Cleophace Kanjagaire ameeleza kuwa kilimo kisichofuata utaratibu wa kitaalam nayo ni sababu inayosababisha katika uharibifu wa mazingira.


Mojawapo ya mikakati iliyowekwa na wadau hao ni pamoja na kupanda miti kwa wingi katika vilima vyote vilivyo wazi,kuacha tabia ya kuchoma moto ovyo,na kufuata ushauri wa wataalam katika kulima na kufuga.

Kwa upande wake afisa mifugo wilaya ya Karagwe Matisera Byenobi amesema kuwa kila kata na kijiji wanatakiwa kutenga maeneo kwa ajili ya kufugia na kubaini wafugaji waliopo na mifugo walioyonayo nah ii ni kutokana na kuwa mifugo nayo inachangia katika uhabifu wa mazingira.
      

About Author

Advertisement

Post a Comment

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top