Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: MKOA WA KAGERA WAVUKA LENGO KATIKA UNDIKISHAJI WA WANAFUNZI AWALI NA DARASA LA KWANZA MWAKA 2018
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
Na: Sylvester Raphael Mkoa wa Kagera wavuka lengo la uandikishaji wa Wananfunzi katika madarasa ya awali na Darasa la kwanza kwa kipin...

Na: Sylvester Raphael

Mkoa wa Kagera wavuka lengo la uandikishaji wa Wananfunzi katika madarasa ya awali na Darasa la kwanza kwa kipindi cha kuanzia mwezi Januari hadi Machi 2018 kipindi cha miezi mitatu na ni kipindi ambacho wanafunzi hupokelewa na kuandikishwa shuleni aidha, ifikapo Machi 31 uandikishwaji hukoma rasmi.


Mkoa wa Kagera kwa mwaka 2018 uliotea kuandikisha wanafunzi wa awali 85,553 wavulana wakiwa 42,678 na wasichana 42,875 lakini mkoa umefanikiwa kuvuka lengo kwa kuandikisha  wanafunzi wa Elimu ya Awali 88,343 wavulana wakiwa 44,66o na wasichana 43,683 sawa na asilimia (103.3%).

Elimu ya darasa la kwanza Mkoa wa Kagera ulilenga kuandikisha wanafunzi jumla 89,043 wavulana 44,686 na wasichana 44,357 ambapo mkoa umevuka lengo kwa kuandikisha jumla ya wananfunzi 96,539 wavulana wakiwa 48,244 na wasichana 48,295 sawa na asilimia (108.42%)



Aidha katika hatua nyingine Mkoa wa Kagera umefanikiwa kuandikisha wanafunzi wa kidato cha kwanza kwa asilimia 90.66 na tayari wanafunzi hao wameripoti shuleni na kuanza masomo yao ya sekondari.Wanafunzi waliofaulu na kuchaguliwa kujiunga na Elimu ya Sekondari wavulana walikuwa 17,191 na wasicha 17,971 jumla 35,161.

Wanafunzi walioripoti katika shule za Sekondari Mkoani Kagera hadi kufikia Machi 31, 2018 jumla ni 31,877  sawa na asilimia 90.66 wavulana wakiwa 14,814 sawa na asilimia 86.173 na wasichana 17,063 sawa na asilimia 94.953.

Mkoa unaendelea na juhudi za kuwafuatilia wanafunzi ambao bado hawajaripoti shuleni kuhakikisha wanaripoti mara moja ili kuendelea na masomo ya kidato cha kwanza. Aidha, uongozi wa Mkoa wa Kagera unatoa rai kwa wazazi na walezi wa wanafunzi ambao bado hawajaripoti shuleni kuhakikisha wanafunzi hao wanaripoti vinginevyo wazazi na walezi watauchukuliwa hatua za kisheria kwa kutowapeleka watoto wao shule.




Vilevile Mkoa wa Kagera unaendelea na juhudi za kuweka mazingira mazuri ya kujifunza na kujifunzia ili kutoa elimu bora kwa wanafunzi. Pia kuhakikisha mkoa unashika nafasi za juu katika mitihani ya kitaifa  na ufaulu wa maksi za juu kama ilivyo desturi ya Mkoa wa Kagera.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top